• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AWATAKA MAAFISA MIPANGO MIJI KUPANGA, KUPIMA NA KUMILIKISHA ARDHI KISHERIA

Posted on: May 30th, 2024

RC MTANDA AWATAKA MAAFISA MIPANGO MIJI KUPANGA, KUPIMA NA KUMILIKISHA ARDHI KISHERIA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka Maafisa Mipango Miji kuhakikisha wanasaidia jamii kupanga, kupima na kumilikisha ardhi kisheria ili kuondokana na migogoro ya ardhi nchini.

Mtanda amebainisha hayo leo Mei 30, 2024 wakati akifungua kikao kazi cha siku mbili cha Maafisa Mipango miji kutoka Mikoa ya Kanda ya ziwa kilichoratibiwa na Bodi ya Usajili wa wataalam wa mipango miji.

Amesema, katika kutimiza hilo ni lazima wajiepushe na rushwa na kuendelea kujifunza zaidi kuhusiana na masuala ya mipango miji ili kuwa na uwezo mkubwa zaidi wa kutafuta suluhu ya changamoto za ardhi hususani ujenzi holela.

Aidha, amemshukuru Rais Samia kwa kutoa fedha nchi nzima kwa ajili ya  kupanga, kupima na kumilikisha ardhi kisheria ili kupata makazi bora kwa jamii na kuondokana na uharibifu wa mazingira kwa kukata miti ya hifadhi na ujenzi holela nchini.

Vilevile, ametoa wito kushirikisha sekta binafsi kushiriki kwenye upangaji wa makazi kwa ajili ya kutafuta fedha kupitia ubunifu wao na Serikali ikaweza kusaidiwa kupata rasilimali fedha hususani kwa kuandaa maandiko yatakayojikita kwenye mipango endelevu.

Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Wataalam hao Dkt. Joel Msami amebainisha kuwa wanao mkakati wa kujenga mifumo nchi nzima kwa ajili ya kusimamia ardhi na majengo na kwamba wanaamini jambo hilo litasaidia kupunguza migogoro ya ardhi nchini.

Msajili kutoka Bodi ya Usajili wa Mipango Miji, Lucas Mwaisaka amesema bodi hiyo ya kitaaluma iliyoanzishwa mwaka 2009 na mpaka sasa imesajili wataalamu 456 pamoja na makampuni kadhaa na kwamba wanaendelea kuyajengea uwezo makundi mbalimbali juu ya masuala ya usajili.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.