• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AWATAKA TAPHATA KUHAKIKISHA WANATOA ELIMU SAHIHI YA MATUMIZI YA DAWA

Posted on: November 26th, 2025

“Kwa mujibu wa ripoti ya benki ya dunia ya mwaka 2018 imeainishwa kuwa, tusipochukua hatua stahiki, ifikapo mwaka 2050 watu zaidi ya milioni 10 watafariki dunia kila mwaka kutokana na magonjwa yatokanayo na vimelea ambavyo vimekua sugu.”.

Ni Rai ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda aliyoitoa leo Novemba 26, 2025 kwa Wateknolojia Dawa na Wateknolojia Dawa Wasaidizi Tanzania (TAPHATA) alipokuwa akifungua Mkutano Mkuu wa 26 wa Chama hicho.

Mkuu wa Mkoa amesema kama wataaluma wa Famasi wana jukumu la kuchukua hatua sasa katika mapambano dhidi ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa.

“Hakikisheni mnatoa elimu sahihi kwa wananchi juu ya matumizi sahihi ya dawa kwa kuwa ninyi ndio kada ya Afya inayohusika zaidi”.

Aidha Mhe. Mtanda ametoa wito kwa Mamlaka na Nabaraza yanayosimamia huduma za dawa na tiba kuhakikisha maduka yote ya dawa yanasajiliwa na kukaguliwa mara kwa mara, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha vituo vyote vya Afya vya umma na binafsi vinavyotunza dawa, vinakua na mtaalamu stahiki wa dawa kwa kuzingatia ikama ya mahali husika.

Sambamba na hayo Mkuu wa Mkoa amesema Changamoto mbalimbali bado zipo, ikiwemo upungufu wa ajira, maslahi katika sekta binafsi, na changamoto za usimamizi wa maduka ya

dawa.


“Nitoe wito kwa Baraza la Famasi na Ofisi ya Mfamasia Mkuu wa Serikali kushirikiana kwa karibu na Chama chenu kusikiliza na kushughulikia changamoto hizi ili taaluma hii iwe na nguvu zaidi na tija kubwa kwa Taifa”.

Aidha Mhe. Mtanda amesema serikali imeendelea kuajiri watalam katika sekta hiyo na kwa mwaka huu serikali kupitia utumishi wameshatangaza ajira zipatazo 10,280 na wateknolojia Dawa wakiwemo.

Nitoe wito wasimamizi wa kada hii kupeleka mapendekezo wizarani ili kuona namna bora ya kuongeza ajira kwa wanataaluma wenu kadri inavyofaa mkiainisha pia maeneo ambayo yana ulazima wa kuwepo kwa wanataaluma kama ilivyosemwa kwenye risala yao. Ameongeza Mkuu wa Mkoa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • STANBIC YAPONGEZWA KWA MSAADA WA VIFAA TIBA MWANZA

    November 27, 2025
  • RC MTANDA AWATAKA TAPHATA KUHAKIKISHA WANATOA ELIMU SAHIHI YA MATUMIZI YA DAWA

    November 26, 2025
  • RC MTANDA AIPONGEZA OFISI YA WAZIRI MKUU KUANZISHA KAMATI ZA MAAFA ZA MIKOA

    November 18, 2025
  • RC MTANDA AWATAKA WATAKWIMU KUTOA TAKWIMU SAHIHI KUCHAGIZA MAENDELEO

    November 18, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.