• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AWATAKA VIONGOZI WA DINI KUIMARISHA MALEZI NA AMANI YA JAMII

Posted on: December 18th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka viongozi wa dini kushiriki kikamilifu katika malezi ya jamii kwa kushirikiana na Serikali, akisisitiza kuwa pande zote mbili ni wachungaji wa watu tofauti ikiwa ni majukumu na maeneo ya utendaji.

Akizungumza leo Desemba 18, 2025, wakati wa kikao na viongozi na wachungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Mashariki ya Ziwa Victoria (DMZV), Mhe. Mtanda amesema wananchi wanaohudumiwa na Serikali ni hao hao wanaohudumiwa na viongozi wa dini.

“Watu ni wale wale isipokuwa kanisani mnawaita waumini, wanapotoka nje kwetu sisi tunawaita wananchi, na wanapokuwa sokoni huitwa wateja au wanunuzi, hivyo hakuna sababu ya kila upande kujitenga katika kuwalea kimaadili”.

Mhe. Mtanda amewataka viongozi wa dini kutekeleza wajibu wao kwa ufanisi mkubwa ili waumini washibe neno la Mungu na kujiepusha na vitendo vinavyokiuka maadili, sheria, kanuni, taratibu pamoja na tamaduni za Watanzania.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa kudumisha amani, ushirikiano kati ya Serikali na taasisi za dini, pamoja na kuimarisha umoja na mshikamano miongoni mwa wananchi kama nguzo muhimu za maendeleo ya Taifa.

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Mkoa amewahimiza viongozi wa dini kuendelea kuliombea Taifa na viongozi wake, akisema maombi ni nyenzo muhimu katika kujenga amani, mshikamano na masikilizano kwa ustawi wa nchi.

“Kwanza kabisa, nawasihi muombe dua, msali na kumshukuru Mungu kwa ajili ya watu wote, kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi maisha ya utulivu na amani pamoja na uchaji wa Mungu na mwenendo mwema”. Amehitimisha Mkuu wa Mkoa kwa kusoma 1 Timotheo 2:1

Akizungumza kwa niaba ya viongozi wa KKKT, Askofu Oscar Itael Lema wa KKKT (DMZV) Mwanza amesema kanisa linaunga mkono juhudi za Serikali katika kujenga jamii yenye maadili na amani.

Amesema kanisa litaendelea kushirikiana na Serikali katika kuwalea waumini kiroho na kimaadili, na kuhakikisha linakuwa chachu ya amani, umoja na mshikamano katika jamii.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • BODI YA BARABARA MWANZA YATAKIWA KUSIMAMIA UBORA NA MATUMIZI SAHIHI YA FEDHA

    January 08, 2026
  • MHE. KUNDO KUKAGUA MIRADI YA MAJI MWANZA KWA SIKU TATU

    January 07, 2026
  • NAIBU WAZIRI CHAYA AITAKA TISEZA KUSIMAMIA UAJIRI WA WATAALAMU KWA WAWEKEZAJI

    January 06, 2026
  • SERIKALI KUPANUA MASOKO YA DHAHABU KIMATAIFA

    January 05, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.