• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AWATAKA VIONGOZI WA DINI KUISAIDIA SERIKALI KUJENGA MAADILI MEMA

Posted on: February 20th, 2025

RC MTANDA AWATAKA VIONGOZI WA DINI KUISAIDIA SERIKALI KUJENGA MAADILI MEMA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka Viongozi wa Dini kulitumia kundi kubwa la Waumini wanaowategemea kuwapelekea habari njema za kiroho ili wawe na utamaduni wa kuwa na matendo mema kwa kutumia imani zao.

Mkuu wa Mkoa ametoa rai hiyo mapema leo tarehe 19 Februari 2025 alipokuwa akitoa salamu katika Mkutano wa Sinodi Kuu (Baraza Kuu la Kanisa la Africa Inland Church Buzuruga Mwanza), ambapo amewataka Viongozi hao kuwakumbusha waumini wao wajibu wa kuishi maisha yenye maadili mema.

“Tukishirikiana vizuri kati ya Serikali na Viongozi wa Dini tutajenga Taifa lenye Watu Waadilifu na hivyo kupunguza kero nyingi zinazoikabili jamii katika

Nchi yetu”. Mhe. Mtanda.

Aidha, Mkuu wa Mkoa amesema uhusiano kati ya Serikali na Dini ni vitu ambavyo havitenganishiki, ni sura mbili za sarafu. Kwa sababu, binadamu ni

mwili na roho na kila kimoja hakina budi kuendelezwa kwani Serikali inashughulika na miili na akili huku Dini zinashughulika na roho.

“Naomba niwahakikishie AICT pamoja na ndugu zetu wanaounga mkono kazi mnazofanya kwamba serikali itaendelea kutoa ushirikiano wa kutosha kwenu ili muweze kutimiza malengo yenu ya kulijenga Kanisa na kuwahudumia Watanzania”.

Kabla ya kuhitimisha hotuba yake Mkuu wa Mkoa amesisitiza kuhusu masula mbalimbali ikiwemo Umoja na mshikamano, kukuza Amani na Utulivu, kuongoza kwa hekima na uwajibikaji, huku akiwataka Viongozi hao wakizingatia maslahi ya jamii yote na kuwahudumia waumini kwa uaminifu na upendo.

Akizungumza Kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Mkoa, Askofu Mkuu wa Kanisa la AICT Mhashamu Baba Askofu Musa Masanja Magwesela, amesema Sinodi Kuu iliyoketi leo inaundwa na Dayosisi 7 yani Dayosiis ya Geita, Mara ukerewe, shinyanga, Tabora, Pwani, na Tanga ambapo wachungaji wote wa Makanisa, Viongozi wa idara, wanawake na vijana wanakutana mara moja kwa miaka miwili ambapo kwa mara ya mwisho  waliketi mwaka 2022.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MWANZA, SIMIYU ZANG'ARA UTAMILIFU DARASA LA SABA KANDA YA ZIWA

    May 30, 2025
  • RAS MWANZA AZINDUA RASMI MRADI WA KUPAMBANA NA UGONJWA WA SELI MUNDU

    May 30, 2025
  • WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAPIGWA MSASA MIKAKATI YA KUTOKOMEZA WATOTO WA MITAANI

    May 29, 2025
  • RAS MWANZA AWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUDUMISHA NIDHAMU NA UFANISI KAZINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.