• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AWATAKA WANANCHI KUTUMIA ILEMELA NYAMA CHOMA FESTIVAL KUKUZA BIASHARA

Posted on: November 16th, 2024

RC MTANDA AWATAKA WANANCHI KUTUMIA ILEMELA NYAMA CHOMA FESTIVAL KUKUZA BIASHARA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo Novemba 16, 2024 amezindua tamasha la Ilemela nyamachoma na amewataka wafanyabiashara kutumia fursa hiyo kukuza mitaji na kipato cha biashara zao.

Amesema wananchi hawana budi kulitumia eneo hilo kujenga mahusiano mema na yenye tija kibiashara na liwe eneo mashughuli kwa nyama choma, vyakula vingine na vinywaji na kupumzika ambapo litasaidia kukuza utalii.

"Huu ni mwanzo, matarajio ni kuboresha zaidi eneo hili na siku za usoni tutakua na nyama choma, muziki mubashara na pombe na Nyamhongolo itakua maarufu kwa shughuli hizi na wageni wakifika Mwanza watajua eneo rasmi ni hapa."

Aidha, amebainisha kuwa uwepo wa shughuli rasmi wakati wote kwenye eneo hilo utasaidia pia kujenga jamii ya Mwanza kimaadili kwa kulitumia eneo hilo kujengana katika makundi mbalimbali ya kijasiriamali.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela Bi. Ummy Wayayu amesema kwa kushirikiana na wadau wataendelea kuboresha eneo hilo na kwamba uwepo wa Nyama choma utasaidia wananchi kupata sehemu ya kupoteza mawazo.

Naye, Mbunge wa Ilemela Mhe. Dkt. Angelina Mabula ametumia wasaa huo kumpongeza Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kwa ubunifu ambao amebainisha kuwa tamasha hilo litasaidia kukuza mapato ya halmashauri.

Aidha miongoni mwa maoni mengi ya wadau wa nyama choma  wameomba kuboreshewa miundombinu ya eneo hilo ili liweze kuwa bora zaidi na vyombo vya habari kuendelea kulitangaza tamasha hilo ili lizidi kuwa kubwa zaidi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.