• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AWATAKA WANUFAIKA WA MRADI WA VIZIMBA KUWEKA UMAKINI KATIKA UWEKEZAJI HUO

Posted on: August 7th, 2024

RC MTANDA AWATAKA WANUFAIKA WA MRADI WA VIZIMBA  KUWEKA UMAKINI KATIKA UWEKEZAJI HUO


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka vijana waliokopeshwa vizimba vya kufugia samaki Kanda ya Ziwa Viktoria hususani Mkoa wa Mwanza kuhakikisha wanaweka umakini wa kutosha katika usimamizi wa uwekezaji huo ili uwaletee manufaa.

Mhe. Mtanda ametoa wito huo leo Agosti 07, 2024 alipotembelea na kukagua maendeleo ya mradi huo  uliotolewa kwa mkopo bila riba kupitia benki ya maendeleo ya kilimo (TADB) kwa makundi maalum ya wanawake, walemavu na Vijana katika mtaa wa Kisoko uliopo Wilayani Nyamagana.

Mkuu huyo wa Mkoa amewataka wanufaika hao kuzingatia pia utunzanji wa kumbukumbu kwa kipindi chote wawapo shambani hapo, aidha ameutaka uongozi wa mahali hapo kuhakikisha wanakuwa na daftari maalumu la wageni ambalo pia watalitumia kuandika maoni yao ili wakija viongozi na wageni mbalimbali watumie daftari hilo katika kutazama na kuona ni kwa namna gani wanaweza wakatatua changamoto au kero zilizoainishwa katika daftari hilo.


"Mali bila daftari huisha bila habari,  ni lazima muwe na daftari la wageni hata kama anakuja DC anakuta mmendika changamoto ya barabara basi yeye atajua ni namna gani ataliwasilisha suala hilo kwa mamlaka husika na changamoto yenu inakua imepata tiba". Mhe. Mtanda.

Kadhalika Mhe. Mtanda amewataka wanufaika hao kuweka umakini wa hali ya juu kwa kuwa na usimamizi bora wa vizimba hivyo kwa kuwa Serikali ya Rais Samia imedhamiria kwa dhati kuwasaidia wananchi wake kujikwamua na umaskini kwa kuwapatia wanufaika hao zaidi ya shilingi bilioni 4 katika uwekezaji huo wa ufugaji wa samaki wa vizimba.

"Msifanye mambo kwa kutania tania, kama mmedhamiria kufanya uwekezaji hapa ziwani basi acheni ubabaishaji kuweni makini katika kusimamia, msipofanya hivyo nyie wapo wageni watakaokuja kuitumia fursa hii vizuri. Ameongeza Mkuu huyo wa Mkoa.

Mkoa wa Mwanza umebahatika kupata wanufaika wengi ambao ni 69 (Vikundi, ushirika  na watu binafsi wenye wanufaika 1305) pamoja na vizimba 255 vya mkopo usio na riba, ambapo kwa eneo la Kisoko pekee vimesanikishwa vizimba 112 na kuna jumla wanufaika 392 kwa awamu ya kwanza na ya pili.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.