• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Mwanza aadhimisha Siku ya Wauguzi Duniani kwa kuhimiza Lishe bora kwa mama na mtoto

Posted on: May 26th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Mhandisi Robert Gabriel ameadhimisha siku ya Wauguzi Duniani akiwataka wakina mama wajawazito kuzingatia kanuni zote za afya ili kulinda afya zao na mtoto.


Akiwa mgeni rasmi katika Maadhimisho hayo yaliyofanyika ki-Mkoa kituo cha Afya Buzuruga Wilayani Ilemela Mkoani Mwanza,Mhe Gabriel amesema Afya ya mama na mtoto itaimarika kwa kuzingatia kufika vituoni ambapo huko atapata tiba sahihi na ushauri wa kitaalam.


"Mama zangu nimefurahi kuwaona hapa natambua leo ni siku yenu ya kuja kupata matibabu na maendeleo ya afya zenu,zingatieni sana lishe bora kuepuka Utapiamlo"


Akiwa kituo cha Afya Buzuruga Mkuu huyo wa Mkoa ametembelea  kuona shughuli mbalimbali za Wauguzi na kuwakumbusha kuzingatia viapo vyao katika utendaji wao wa kazi wa kila siku.


Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza,Dktr Thomas Rutachunzibwa amesema Wauguzi ndiyo uti wa mgongo katka Sekta ya Afya hivyo amewakumbusha kufanya kazi kwa kuzingatia viapo vyao wakati Serikali ikiendelea kuzifanyia kazi changamoto za mazingira yao ya kazi.

Naye Makamu wa Rais wa Chama cha Wauguzi nchini TANNA, Ibrahim Mgoo ameiomba Serikali kuendelea kuwekeza kwa Wauguzi kwa kuwajengea uwezo ikiwemo kuwaendeleza kitaaluma.

Kwa upande wake Katibu wa Chama cha Wauguzi Mkoa wa Mwanza,Martha Mkinga amesema bado muuguzi mmoja anawahudumia wateja kuanzia 20 hadi 30 badala ya 6 hadi 8 wanaendelea kuamini Serikali itaifanyia kazi changamoto hiyo.

Maadhimisho ya siku ya Wauguzi Duniani Kitaifa yamefanyika  Mei 22 mwaka huu Mkoani Kilimanjaro kauli mbiu yake ikiwa ni WAUGUZI SAUTI INAYOONGOZA WEKEZA KWENYE UUGUZI NA HESHIMU HAKI KULINDA AFYA KWA WOTE.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MAKUZI YA AWALI YA MTOTO MSINGI WA UJENZI WA TAIFA IMARA - RAS BALANDYA

    May 16, 2025
  • RC MTANDA AWAKARIBISHA MWANZA WANAFUNZI KUTOKA UGANDA

    May 15, 2025
  • RC MTANDA AKOSHWA NA BONANZA LA USHIRIKA NA MABENKI

    May 14, 2025
  • RAS MWANZA ATAKA UHAMASISHAJI CHAKULA CHENYE LISHE KUONGEZEKA SHULENI

    May 13, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.