• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC-MWANZA Azindua Chanjo ya Matone ya Polio Ukerewe

Posted on: May 18th, 2022

Mkoa wa Mwanza umepanga kuhakikisha inatoa chanjo kwa watoto 846,733 na imejipanga katika vituo 355 ambapo jumla ya watoa huduma 6,909 wamepata mafunzo kwa ajili ya kutoa huduma hiyo.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Mhandisi Robert Gabriel leo Mei 18,2022 alipokuwa akizindua  Chanjo ya matone ya Polio katika kituo cha Afya Nakatunguru kilichopo Wilaya ya Ukerewe mkoani Mwanza.

 "Ukerewe ina jumla ya wakazi 518,114 kati yao watoto wenye umri wa chini ya miaka 5 ni 108,937 ambao ndiyo lengo la chanjo ya Matone ya Polio," amesema Mhandisi Robert Gabriel.

Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt. Thomas Rutachunzibwa amesema,tulizoea kufanya shughuli hizi za uzinduzi makao makuu ya Mkoa na kuahidi kuwa  ni mwanzo wa kufanya Shughuli za kimkoa na nyingine zitaendelea kufanyika Wilayani hapa.

"Kampeni hii itafanyika kwa siku 4 kuanzia tarehe 18 hadi 21 Mei 2022 ambapo lengo ni kuchanja watoto 846,733 katika Mkoa Mzima kwa Wilaya ya Ukerewe inatakiwa kuchanja watoto 108,937."

Dkt.Rutachunzibwa ameongeza kuwa Chanjo zitatolewa kupitia vituo 355 vikiwemo vituo 38 vya Wilaya ya Ukerewe na Watoa huduma 6,909 wamepata mafunzo kwa ajili ya kazi ya Uchanjaji,Watunza takwimu na wahamasishaji.

"Tumesambaza chanjo Dozi 973,740 katika vituo vyote na maandalizi ya kutoa chanjo hiyo yamekamilika na chanjo hii inatolewa bila malipo.

Naye Diwani wa kata ya Nakatunguru,Mataba Sosthenes ameshukuru kwa uzinduzi wa kampeni ya Polio katika kata yao na  amemuomba Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe Mhandisi Robert Gabriel kuwasadia katika maboresho ya huduma mbalimbali katika kituo cha afya cha Nakatunguru.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.