• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RMO MWANZA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI VITUO VYA AFYA NA ZAHANATI SENGEREMA

Posted on: December 29th, 2025

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dkt. Jesca Lebba leo Desemba 29, 2025, amefanya ziara maalum ya kikazi Wilaya ya Sengerema kwa lengo la kukagua vituo vya afya na zahanati zinazoendelea na ujenzi pamoja na zile zinazotoa huduma kwa jamii ili kujiridhisha na utendaji kazi na ubora wa huduma za afya zinazotolewa kwa wananchi.

Dkt. Lebba ametembelea jumla ya vituo vitano ambavyo ni Zahanati ya Tabaruka, Ngoma B na Nyalwambu pamoja na Vituo vya Afya vya Kaomolo na Kamanga, ambapo amekagua maendeleo ya ujenzi, upatikanaji wa huduma na mazingira ya utoaji huduma kwa wananchi.

Akiwa katika ziara hiyo, amewataka mafundi na wasimamizi wa miradi kuongeza kasi ya ujenzi ili vituo hivyo vikamilike kwa wakati na kuanza kutoa huduma kwa jamii.

Hata hivyo, amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema kuhakikisha vituo ambavyo bado havijakamilika vinakamilishwa kwa kuzingatia muda uliopangwa.

Aidha, Dkt. Lebba amemshukuru Mhe. Rais Dr. Samia suluhu Hassan kwa kuendelea kufanya uwekezaji mkubwa katika sekta ya afya hususani katika miundombinu, vifaa tiba, bidhaa za afya pamoja na kuongezeka kwa idadi ya watumishi wa afya, jambo linalochangia kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi na hii ni utekelezaji wa bima ya afya kwa wote ndani ya siku 100 kwa kuhakikisha vituo vya huduma za afya vinakamilika na kuanza kutoa huduma bora.

“Uwekezaji mkubwa umefanyika upande wa miundombinu, vifaa tiba, bidhaa za afya kwa ujumla pamoja na watumishi, na ndio maana tunaweza kuwagawa katika maeneo mbalimbali ya utendaji kazi,” amesema Dkt. Lebba.


Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema, Dkt. Darison Andrew, amesema kuwa upatikanaji wa dawa umefikia asilimia 95.2%, wahudumu wa afya wanapatikana na huduma zinaendelea kutolewa kwa ufanisi, huku baadhi ya vituo vikiendelea kufanyiwa maboresho.

Hata hivyo amepongeza ujio wa Mganga Mkuu wa Mkoa na kuahidi kuyafanyia kazi maelekezo yote yaliyotolewa, kwa lengo la kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora, salama na zenye viwango vya juu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA UMWAGILIAJI IBANDA–IGAKA WA BILIONI 35 HAUTASIMAMA – SILINDE

    January 10, 2026
  • RC MTANDA MGENI RASMI MECHI YA KIRAFIKI SIMBA VS PAMBA MWANZA

    January 10, 2026
  • BODI YA BARABARA MWANZA YATAKIWA KUSIMAMIA UBORA NA MATUMIZI SAHIHI YA FEDHA

    January 08, 2026
  • MHE. KUNDO KUKAGUA MIRADI YA MAJI MWANZA KWA SIKU TATU

    January 07, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.