• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RMO MWANZA ATAKA UBUNIFU KUFIKISHA ELIMU YA MALEZI, MAKUZI KWA JAMII

Posted on: August 19th, 2025

Mganga Mkuu Mkoa wa Mwanza Dkt. Jesca Lebba ametoa wito kwa wadau wa Malezi mkoani humo hususani wajumbe wa mkakati wa kutokomeza ukatili wa kijinsia kuwa wabunifu katika kuhakikisha wanafikisha elimu hiyo kwa jamii kwa ajili ya ustawi wa jamii.

Ametoa wito huo mapema leo Agosti 19, 2025 wakati akifungua mkutano wa maandalizi ya kikao cha malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto kitakachofanyika mapema mwezi Septemba 2025 chini ya uongozi wa Katibu Tawala wa Mkoa.


Amewataka wadau hao kuhakikisha wanatumia fursa ya ratiba ya wizara ya mwezi huo wa uelimishaji unaoambatana na wiki ya ustawi wa jamii kwenda kutoa elimu kwenye jamii kwa kutumia mbinu mbalimbali kama redioni na mikusanyiko vijijini kuhusiana na malezi na ukatili wa kijinsia kabla ya kuchukua sheria kwa wakaidi.

Amesema serikali imeweka afua tano kuhakikisha makuzi, malezi na maendeleo ya mtoto yanakua na ustawi na kwamba programu mbalimbali zinazosawili afua hizo yanapaswa kuzingatiwa kwa gharama yoyote ili mwisho wa siku jamii iwe salama.

Vilevile, ametumia wasaa huo kuwashukuru wadau wote pamoja na kumpongeza Afisa Ustawi wa Jamii wa Mkoa pamoja na wasaidizi wake kwa uchapakazi kwani Mwanza imepiga hatua kubwa katika kuelimisha na kupunguza matendo ya ukatili kutokana na juhudi zao za kuhakikisha elimu ya malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto inawafikia wananchi.

Akitoa salamu za Wizara ya maendeleo ya Jamii Idara ya Mtoto bi. Mery Shila amesema wizara hiyo kwa kushirikiana na mikoa wanahakikisha mtoto kuanzia mwaka mmoja hadi minane analindwa na jamii nzima na ndio maana wanasukuma afua mbalimbali za malezi.

Aidha, amebainisha kuwa viongozi wa dini kote nchini wamekua kiungo kikubwa kwenye malezi ya watoto kwa kutoa malenzi na mafundisho ya kiroho katika kuhakikisha wanakua na tabia njema ili ikiwezekana madawati ya jinsia yakose mashauri ya ukatili.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RMO MWANZA ATAKA UBUNIFU KUFIKISHA ELIMU YA MALEZI, MAKUZI KWA JAMII

    August 19, 2025
  • ASASI ZA KIRAIA ZATAKIWA KUTOFADHILI UGAIDI

    August 19, 2025
  • KAMATI YA MTAKUWWA MWANZA YATAKIWA KUTIMIZA WAJIBU WA KULINDA JAMII DHIDI YA UKATILI

    August 13, 2025
  • ZAIDI YA WALENGWA ELFU HAMSINI WANUFAIKA NA RUZUKU YA BILIONI 82 MWANZA

    August 13, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.