• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

SAUT- Yaaswa kusajiri kikundi chao Kisheria

Posted on: March 8th, 2018


Umoja wa wanawake wanafunzi katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino Mwanza –SAUT wameaswa kusajiri kikundi hicho kisheria ili waweze kufaidika na fursa mbalimbali za kiuchumi katika kuelekea uchumi wa viwanda na malengo ya maendeleo ya Dunia ya Milenia.“Millennium Development Goals”.

Haya yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella wakati wa maadhimisho ya  siku ya wanawake duniani yaliyofanyika katika Ukumbi wa M10 Chuoni hapo, akiwa ni mgeni Rasmi katika Jumuiya ya Chuo hicho,Kampasi ya Malimbe Jijini Mwanza ambapo kwa mwaka huu kauli mbiu ya maadhimisho hayo kitaifa ni KUELEKEA UCHUMI WA VIWANDA,TUIMARISHE USAWA WA JINSIA NA UWEZESHAJI WA WANAWAKE VIJIJINI.

Akihutubia katika maadhimisho hayo Mhe. Mongella amewataka washiriki wote wa maadhimisho hayo kujiuliza maswali yenye kuleta dhana nzima ya siku ya wanawake, “Nini maana ya siku hii, ilianzishwa na nani, ilianzishwa kwa sababu zipi,Je wadau wa maendeleo hususani Taasisi za Elimu ya juu kama SAUT kupitia tafiti mbalimbali zinasaidiaje jamii ya akina mama, na zinamuhusishaje mwanamke aliyeko kijijini kuijua dhana nzima ya Uchumi wa Viwanda Tanzania”.Alisema Mhe.Mongella.

Mhe. Mongella amesisitiza kuwa zaidi ya kusherekea mafanikio na jitihada za kuleta usawa wa kijinsia katika familia, katika jamii, na katika taasisi zetu tunao wajibu wa kutumia muda kutafuta fursa na kutafuta majibu ya changamoto mbalimbali katika jamii ili kuendelea kubomoa ukuta unaokwamisha wanawake kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo.

Aidha, amefurahishwa na ushirikiano uliopo kati ya Chuo kikuu cha SAUT na Shule za Sekondari ambazo ni majirani na Chuo hicho katika Mkoa wa Mwanza hali inayotia hamasa hususani kwa vijana walioko Sekondari kuuona umuhimu wa kuifikia elimu ya juu, ambapo Sera ya Awamu ya tano ni “kuelekea uchumi wa viwanda” na vijana ndio tegemeo la nguvu kazi ya uzalishaji kupitia viwanda vyetu tunavyoviandaa hivyo ameahidi Serikali ya Mkoa kuendelea kutoa ushirikiano katika suala zima la ulinzi na usalama,na shughuli nyinginezo za kimaendeleo.

Mhe.Mongella ameawahidi kuwashirikisha hususani wanawake katika fursa zitakazijitokeza katika ofisi yake na wadau wa maendeleo ya wanawake Kitaifa na Kimataifa,pia amewataka kuwa wabunifu wa miradi na shughuli zinazowalenga wanawake vijijini kwa kuwaelimisha na kuwashirikisha kupitia dhana ya usawa kwa mpango wa huduma kwa jamii.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.