• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Sera ya Makazi,Sera ya Taifa ya nyumba Yajadiliwa kuboresha mapendekezo

Posted on: September 16th, 2019


 Katibu tawala Mkoa wa Mwanza Christopher Kadio ameongoza kikao cha sera ya Taifa ya Maendeleo ya Makazi na Sera ya Taifa Ya Nyumba kwa niaba ya Mkuu wa Mkuu wa Mkoa Mhe.  John Mongella ambaye ndiye alikuwa mgeni rasmi katika kikao hicho.

Akiongea katika kikao hicho chenye lengo la kujadili sera  ya mapendekezo ya makazi na sera ya Taifa ya nyumba  Kadio amebainisha kuwa takwimu zinaonyesha asilimia 75% ya wakazi wanaoishi mijini wanaishi kwenye makazi holela na kwamba makazi hayo yana upungufu wa miundombinu na huduma zingine za kijamii.

"Takwimu za watafiti zinaonyesha wakazi zaidi ya asilimia 75% mijini wanaishi kwenye makazi holela au yasiyopangwa, makazi hayo yana upungufu mkubwa wa miundombinu na huduma zingine za kijamii. '' Alisema kadio.

Pia, kadio ameeleza kuwa warsha za kuwasilisha sera zilizopitiwa na wizara ya ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi zitawasilishwa kila kanda na kuwa maamuzi hayo ya kuwasilisha na kupata mchango kutoka kwa wadau yanaonyesha umuhimu wa wadau katika jukumu la kuhakikisha taifa letu lina sera zinazoainisha maisha ya baadae ya watanzania.


"Maamuzi ya kuwasilisha na kupata mchango wa wadau kutoka kanda zote za wizara yanaonyesha umuhimu wa sera hizo kitaifa pamoja na nafasi muhimu ya wadau katika jukumu la kuhakikisha kuwa taifa letu lina sera zinazoainisha maisha halisi ya lengo la mategemeo ya baadae ya watanzania. "


Naye Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana,  Dkt. Phillis Nyimbi,  amesema kuwa  kuwepo kwa warsha ya kuwasilisha sera zinazoandaliwa ina tija katika mkoa wa Mwanza kwani amekuwa akikutana na migogoro mingi ya ardhi, vile vile na makazi ambayo ni holela.

"Kuwepo kwa warsha hii ya kuwasilisha sera zinazoandaliwa ina tija kubwa sana kwa Mkoa wa Mwanza kwani kama kiongozi nimekuwa nikikutana na migogoro mingi sana ya ardhi, na makazi mengi ambayo ni holela," Alisema Dkt. Nyimbi.

Akizungumza katika kikao hicho Muhadhiri Mwandamizi Chuo cha Ardhi Prof. Wilbard Kombe amesema kuwa kunapokuwa na makazi bora kunawasaidia watu wa kima cha chini kuzalisha kipato na kupata nafuu ya kuishi maisha yao, lakini pia kunaleta mabadiliko katika taifa na kuweza kufikia uchumi wa kati.

"Kuwepo kwa nyumba hasa kwa watu wa kima cha chini ndiyo mahali watu wanazalisha kipato na kupata nafuu ya kuishi maisha yao,"alisema Prof. Kombe.

Naye mtafiti kutoka chuo cha Ardhi,  Dkt. Tatu Limbumba  amebainisha kuwa asilimia kubwa ya watanzania wanaishi katika nyumba za kupanga, makazi duni kwa kuhofia kuchukuwa mikopo kutoka katika mashirika tofauti kwani hali zao za uchumi ni duni.  

"Chunguzi nyingi zimebaini kuwa asilimia 50 ya binadamu tunaishi nyumba za kupanga, makazi duni, nyumba zilizojengwa na mafundi wasio na ujuzi, na changamoto kubwa ni idadi kubwa ya watanzania wanaogopa kukopa pesa au nyumba katika mashirika tofauti tofauti kuhofia hali ya uchumi waliyonayo," Alisema Dkt. Tatu.

Pamoja na hayo  Kadio amewataka wadau wote wa kikao hiki kuwa watakapo ondoka wakafikishe madhumuni   ya kikao hicho  katika jamii na sehemu wanazofanya kazi na kusema kuwa huu ni wajibu unawahusu viongozi wote, watumishi wa umma, taasisi binafisi na za serikali, vile vile amewasihi wadau hao kushiriki kikamilifu katika kufuatilia mawasilisho ya wataalamu na kutoa hoja zinazosaidia kuboresha sera hizo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.