• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

SERIKALI INATAMBUA MCHANGO WA WALIMU KATIKA UJENZI WA TAIFA - RC MTANDA

Posted on: December 16th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesisitiza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inathamini mchango wa walimu katika ujenzi wa Taifa.

Akizungumza katika hafla ya kikao cha Watumishi wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) Mhe. Mtanda ameeleza kuwa kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI, serikali imefanya maboresho makubwa katika maslahi na mazingira ya kazi ya walimu.

“Mafanikio haya yanajidhihirisha katika kuongezeka kwa ajira za walimu kila mwaka. Hivi sasa usaili unaendelea katika maeneo mbalimbali ya nchi, ambapo walimu 1,168 wameajiriwa mkoani Mwanza kuanzia mwaka 2021,” amesema Mhe. Mtanda.

Aidha, amebainisha kuwa serikali imeongeza juhudi katika kuboresha miundombinu ya shule, kulipa madeni ya walimu kwa wakati, na kuanzisha mifumo ya kidijitali inayorahisisha huduma kwa watumishi wa umma.

Miongoni mwa mafanikio mengine, serikali imefanikiwa kugawa zaidi ya vitabu milioni 6.1 kwa shule za msingi na sekondari, ili kuboresha ufundishaji na ujifunzaji.

Kwa upande mwingine, Mhe. Mtanda amesisitiza kuwa licha ya changamoto zilizopo, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kuwa mstari wa mbele kuhakikisha upatikanaji wa rasilimali za kifedha na watu kwa ajili ya maendeleo ya sekta ya elimu nchini.

Katika kipindi cha 2021-2025, Mkoa wa Mwanza umepokea zaidi ya shilingi 96 bilioni kwa ajili ya elimu bila malipo, ikilinganishwa na TSh. bilioni 65 zilizotolewa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2017/2018 hadi 2020/2021.

Mhe. Mtanda amemalizia kwa kuwataka walimu kuwa na mshikamano katika chama chao, akisema, “Umoja ni nguvu, utengano ni udhaifu. Tuwe na umoja ili kuendeleza malengo yetu ya kuboresha sekta ya elimu.”

Huu ni uthibitisho wa dhamira ya serikali katika kuboresha sekta ya elimu na kuwaheshimu walimu, ambao ni nguzo muhimu katika maendeleo ya taifa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WAHITIMU AFYA WAASWA KUTUMIA ELIMU KUCHOCHEA MABADILIKO YA JAMII

    December 21, 2025
  • WAHITIMU AFYA WAASWA KUTUMIA ELIMU KUCHOCHEA MABADILIKO YA JAMII

    December 21, 2025
  • MIUNDOMBINU YA MICHEZO ISIWE YA KIBINAFSI- RC MTANDA

    December 21, 2025
  • MIUNDOMBINU YA MICHEZO ISIWE YA KIBINAFSI- RC MTANDA

    December 21, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.