• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Serikali ya awamu ya Sita kufanya mageuzi makubwa Sekta ya Elimu nchini.

Posted on: April 25th, 2023


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe.Prof. Adolf Mkenda amesema Serikali ya awamu ya Sita inaendelea kufanya mageuzi makubwa katika sekta ya elimu ikiwemo kuandaa walimu  watakaokidhi soko la ajira wanaosoma katika vyuo 35 vya ualimu  vilivyopo nchini.

Pia Serikali inaendelea kuboresha mazingira ya ujifunzaji na ufundishaji katika ngazi zote za elimu kuanzia  Msingi, Sekondari, Vyuo vya kati na  Elimu ya juu ili kuleta tija kwa wahitimu wawapo katika soko la ajira.

Mhe.Prof.Mkenda amebainisha hayo leo Aprili 25,2023  jijini Mwanza wakati akizungumza na wadau wa elimu kabla hajazindua mradi wa ujenzi wa jengo la Maktaba na Maabara za Sayansi na Tehama  katika Chuo cha Ualimu nchini ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 59 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

"Maelekezo ya Mhe. Rais  wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Samia Suluhu Hassan ni kwamba wanafunzi wakihitimu waweze kujiajiri  anachotaka ni elimu yetu hapa nchini  iongeze ujuzi kwa vitendo," amesema Mhe.Prof.Mkenda.

Akizungumzia miaka 59 ya Muungno wa Tanganyika na Zanzibar itakayoadhimishwa kesho April 26 2023, Prof.Mkenda amewaasa vijana wanaosoma vyuoni wasimamie muungano huo bila kuyumba, kutetereka na kubabaika ili kuwaenzi waasisi wa nchi hii.

"Chuo hiki kimeanza mwaka 1939 hadi leo vijana kutoka sehemu balimbali nchini wanakuja hapa kusoma hii ni kutokana na amani na utulivu iliyopo katika nchi yetu ambayo ni matunda ya waasisi wa nchi hii hivyo tusimame kidete kuutetea na kuulinda kwa kila hali muingano wetu,"

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Adam Malima amesema kwa kipindi cha mwaka 2020/2021 na 2021/2022 Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dk.Samia Suluhu Hassan  imeimarisha Elimu ya Ualimu kwa kupeleka fedha katika vyuo vya Ualimu kwa ajili ya mafunzo ya walimu tarajali na mafunzo kazini kwa watumishi.

 "Kupitia uimarishaji huo Chuo cha Ualimu Butimba kwa kipindi cha mwaka 2020/2021 na 2021/2022 kilipokea  zaidi ya Sh bilioni moja kwa ajili ya Ujenzi wa Maabara za Fizikia, Kemia Maabara ya Tehama, Vyumba vinne vya madarasa, Ukumbi wa mihadhara na kukarabati majengo ya Maabara ya Baiolojia na Maktaba.

"Pia katika kipindi cha mwaka 2021/2022 na 2022/2023 Serikali ya awamu ya sita ilileta fedha katika chuo hiki kiasi cha Sh milioni 715,163,287.28 kwa ajili ya kugharamia Mafunzo ya Ualimu kwa vitendo, mafunzo hayo hutoa fursa kwa wa wanachuo kupata tajiriba ya kumudu Maisha ya kazi na uhalisia wa Mazingira ya kazi, " amesema Mhe.Malima na kuongeza

"Pamoja na kujenga majengo ya miundombinu ya Chuo Kipya cha Murutunguru kilichopo Wilaya ya Ukerewe Mkoani Mwanza kwa kipindi cha mwaka 2020/2021 hadi 2023 Serikali imepeleka fedha zaidi ya Sh milioni 369 kwa ajili ya kujenga bweni la wasichana lenye uwezo wa kuhudumia watumiaji 80 na vyumba vinne vya madarasa vyenye uwezo wa kuhudumia watumiaji 200 kwa wakati mmoja," ameeleza Mhe.Malima.

Akisoma taarifa ya mradi wa Ujenzi na Ukarabati wa Majengo ya Maabara za Sayansi, Tehama na Maktaba kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Prof.Carolyne Nombo, Mkurugenzi Msaidizi Ualimu wa Wizira hiyo, Bwana Huruma Mageni amesema mradi huo umetekelezwa kupitia mradi wa kuendeleza Elimu ya Ualimu (TESP) kwa  gharama ya Sh Milioni 467,695,598.00.



Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.