• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Serikali Yaazimia kuinua ufaulu Shule za msingi 2019/2020

Posted on: August 17th, 2019


Serikali imetoa maazimio 14 kwa  walimu wakuu, maofisa elimu wa kata na taaluma ambayo wanapaswa kuyatekeleza kiukamilifu kwa lengo la kuinua ufaulu kwa shule za msingi 2019/2020.

Maazimio hayo yalifikiwa  katika kikao kilichofanyika  jijini Mwanza kati ya Afisa elimu mkoa na wakuu wa shule, maafisa elimu kata na taaluma ambapo ilibainika zaidi ya wanafunzi 1,034 hawakufanya mtihani wa ukamilifu ‘mock’ ngazi ya mkoa, idadi ambayo ilielezwa ni kubwa sana.

Akizungumza na waandishi wa habari, Afisa Elimu Mkoa wa Mwanza, Michael Ligola alisema katika majadiliano ya pamoja wamebaini sababu kadhaa ambazo kwa namna moja au nyingine zinashusha taaluma na ufaulu.

Alisema kutokana sababu hizo, kama Serikali ya mkoa imeelekeza  walimu wakuu, maafisa elimu kata na taaluma kutekelezwa maazimio 14  kuanzia sasa na matokeo yake yatapimwa kuanzia  ufaulu wa mtihani wa kuhitimu darasa la saba 2019.

“kwanza tumewataka walimu wakuu kuacha migogoro na walimu wengine, pia wanapaswa kukaa na wazazi ili kurahisisha utendaji kazi,  walimu wakuu kutoa motisha kwa walimu wanaojituma na bidii zao zinaonekana. Walimu wakuu waipende kazi yao na kuongeza juhudi na maarifa ya usimamizi na ufuatiliaji taaluma.

“maofisa elimu kata na walimu wakuu kuhakikisha wanashirikiana na watendaji wa kata na vijiji kuthibiti utoro, kuongeza  utoaji wa majaribio darasani kwa kutumia mitihani iliyopita, kuhamasisha  wanafunzi wapate chakula shuleni.

“Walimu wakuu kutambua watoto wenye uwezo mdogo katika somo la hisabati na kuwasaidia maswali  kuazia  swali la 1-25 kwa vitendo, walimu bingwa kuongeza bidii katika darasa la saba, kuanziasha   ufundishaji shirikishi  kwa kujadiliana mada ngumu ili kuongeza uelewa, mwalimu mkuu kupunguza safari na vikao nje ya kituo cha kazi,”alisema.

Ligola alisema maazimio mengine ni walimu wakuu kuhimiza ufundishaji wa kusoma, kuhesabu na kuandika (K.K.K) katika darasa la kwanza na la pili,  walimu kuwa na upendo kwa wanafunzi na kuwajenga kisaikolojia kwa kuwaondoa woga, wazazi waelimishwe umuhimu wa kusomesha watoto wa kike na sio kuwafanya kama  kitega uchumi.

Wakati wa ufunguzi wa kikao hicho, iligundulika  wanafunzi 1,034  hawakuonekana katika vyumba vya mtihani wa ukamilifu  mock’ mkoani Mwanza.Pia kikao hicho kilikusudia kupata majibu kutoka kwa maafisa elimu na wakuu wa shule sababu ya baadhi ya halmashauri kutofikia asilimia 90 ya ufaulu ambao ni lengo la mkoa huo.

Kwa mujibu wa takwimu za mkoa  huo zinaonyesha  halmashauri ya Ilemela ilifikia asilimia 98.3,  Sengerema 97.1,  Misungwi 96.6, Jiji la Mwanza 95.2, Magu 92, Ukerewe 85.4, Kwimba 84.6 na Buchosa 80.5.

Ligola alisema lengo ni kuona  kuweka mikakati na kutatua changamoto  zilizopo ili kila halmashauri iweze kufikia  asilimia 90 ya ufaulu katika mitihani ya kitaifa. Ligola alisema Julai 17-18 mwaka huu kulifanyika mtihani wa mjaribio mkoa ambapo wanafunzi 68,356 kutoka shule za msingi 944  walitarajiwa kufanya  lakini  waliongia vyumbani  siku hiyo ni  67,322 kati ya hao wavulana  31,789 mna wasichana 35,533 na asilimia 98.3.

Alisema wanafunzi ambao hawakufanya mtihani huo  1,034 kati ya hao wavulana ni 347 na wasichana 687 sawa na silimia 1.5, hivyo alisema kiwango hicho cha wanafunzi wasiofanya mtihani ni kikubwa na kinapaswa kutafutiwa suluhisho.

“Lengo la Serikali ni ufaulu uwe asilimia 100 kitaifa lakini hapa Mkoa wa Mwanza tulijiwekea malengo yetu yawe asilimia 90 au zaidi,sasa katika  mitihani ya majaribio tuliyofanya ngazi ya mkoa baadhi ya halmashauri zimeonekana kutofikia lengo letu, sasa nimelazimika kuwakutanisha ili kila mmoja aseme kilichomkwamisha hali hiyo kujitokeza.











Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.