• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

SERIKALI YABORESHA HUDUMA ZA SARATANI YA MATITI MWANZA

Posted on: October 22nd, 2025

Serikali kwa kushirikiana na Shirika lisilo la Kiserikali la Jhpiego imeendelea kuboresha huduma za matibabu ya saratani ya matiti Mkoani Mwanza kupitia Mradi wake wa Beat Breast Cancer awamu ya pili unaodhaminiwa na PFIZER Foundation ambao unalenga kupunguza vifo vinavyotokana na ugonjwa huo kwa kuimarisha uchunguzi wa mapema na upatikanaji wa matibabu.


Akizungumza leo Oktoba 22, 2025 na waandishi wa habari ofisini kwake, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dkt. Jesca Lebba ameipongeza serikali kwa hatua hiyo muhimu na kuishukuru kwa kuuchagua Mkoa wa Mwanza kuwa miongoni mwa wanufaika wa awamu ya pili ya mradi huo.


Dkt. Lebba amewataka wananchi wa Mkoa wa Mwanza kuchangamka kwa kujitokeza kwa wingi katika vituo vya kutolea huduma za afya ili waweze kuchunguza afya zao na kupatiwa matibabu.

“Tutahakikisha tunawafikia wananchi wa maeneo yote na nitoe rai kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kuja kuchunguza afya zao na kupatiwa huduma za uchunguzi, ushauri na matibabu”.


Ameongeza kuwa changamoto kubwa ambayo wanakutana nayo ni uelewa mdogo wa jamii juu ya dalili na matibabu ya saratani ya matiti, watoa huduma wachache pamoja na vituo vya kutolea huduma hiyo ya vipimo na elimu juu ya ugonjwa huo.


Aidha, amesema wameweza kufanya uchunguzi kwa wanawake zaidi ya 23,000 na kuanzia mwezi Januari mpaka Septemba mwaka huu wananchi 46 wamebainika kuwa na saratani ya matiti na kati yao 27 wameshaanza kupatiwa matibabu na wengine wapo katika ushauri nasaha.


Naye Daktari Bingwa wa Upasuaji kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Sekou-Toure Dkt. Jackson Chiwaligo amewasisitiza wanawake kujifanyia uchunguzi wa awali ili waweze kutambua mabadiliko katika miili yao, huku akitoa wito waweze kufika hospitali pale ambapo watahisi mabadiliko yoyote katika matiti.

Mkoa wa Mwanza ni miongoni mwa Mikoa minne kwa Tanzania bara ambayo inanufaika na mradi wa PFIZER-BREAST CANCER na kutoa huduma ya kupima na kutibu saratani ya matiti ukiwa na vituo 32 zikiwemo Hospitali ya Kanda, Hospitali ya Rufaa, Hospitali za Wilaya na Halmashauri huku ikifanikisha kutoa elimu kwa watoa huduma 60.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA AIPONGEZA OFISI YA WAZIRI MKUU KUANZISHA KAMATI ZA MAAFA ZA MIKOA

    November 18, 2025
  • RC MTANDA AWATAKA WATAKWIMU KUTOA TAKWIMU SAHIHI KUCHAGIZA MAENDELEO

    November 18, 2025
  • RAS MWANZA AONGOZA WAOMBOLEZAJI MAZISHI YA ALIYEKUWA MTUMISHI WA MWAUWASA

    November 14, 2025
  • MWANZA YASHIRIKI MAFUNZO KUKUZA USAWA WA KIJINSIA NCHINI MKOANI MOROGORO

    November 13, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.