• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Serikali yawaahidi fidia sahihi Wakazi wa Satto na Nyabili Wilayani Sengerema kupisha shughuli za Mgodi

Posted on: June 9th, 2022

Serikali imewahakikishia stahiki zao za fidia kulipwa kwa usahihi na mapema Wananchi wa Vijiji vya Sotta na Nyabila vilivyopo Wilayani Sengerema Mkoani Mwanza ambao wanafanyiwa tathmini ya mali zao kupisha shughuli za Mgodi wa Madini.


Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dktr Angelina Mabula akiongozana na Viongozi  wengine waandamizi wa Serikali amefanya mkutano wa hadhara kuzungumza na Wananchi hao baada ya baadhi yao kushindwa kupata ufahamu sahihi dhidi ya maeneo hayo na zoezi la tathmini kwa ujumla.


Mhe Mabula amesema kwa mujibu wa Sheria ya Ardhi ya mwaka 97 hakuna mtu anayeweza kumiliki maeneo ya Milima,Maziwa,Mito au sehemu za Bahari hivyo ni vyema Wananchi watambue  ili kuepusha migogoro isiyo na tija.

"Nimelazimika kuja kuwapa ufafanuzi huu na kuwaondolea shaka baadhi yenu katika zoezi zima la fidia ambalo kabla Mtathmini Mkuu wa Serikali,Everyn Magasha amelikamisha na hekari moja mtalipwa Shilingi Milioni 2 ikiwa ni nyongeza kutoka Milioni 1.5 ambayo ndiyo bei  ya soko la radhi hii" Mhe Mabula.


Amesema Serikali ya Mhe Rais Samia Suluhu Hassan katika kupigania kuinua Uchumi wa Nchi na Mwananchi imeweka mazingira mazuri kwa Wawekezaji wanaokuja hivyo kazi iliyopo ni kumpa nafasi Mwekezaji huyo aanze kazi mapema iwezekanavyo.


Naibu Waziri wa Madini Dktr Steven Kiruswa amesema tayari Serikali imeshaingia mkataba na Mwekezaji huyo ambaye tayari ametumia Shilingi Bilioni 240 kwa shughuli za Maendeleo ikiwa ni utekelezaji wa yaliyomo ndani ya Mkataba huo.


Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Ngusa Samike amesema hii ni fursa nyingine ya kuwainua kiuchumi  Wananchi wanaoishi jirani na Mgodi huo wajibu wao sasa ni kuiunga mkono Serikali ya Awamu ya Sita ambayo ni Mmbia na Mwekezaji huyo.


Asilimia 85 tayari wameshiriki zoezi la kufanyiwa tathmini ya mali zao kabla ya kulipwa fidia huku asilimia 15 wakiwa bado kutokana na kutopata ufahamu wa kuhusu fidia zao  ambapo sasa wamesha elimishwa na wanatarajiwa kuthaminishwa maeneo yao.

Fidia nyingine watakazo lipwa Wananchi hao ni pamoja na Nyumba,Makaburi,Mazao  stahiki,Posho ya kusafirisha mizigo tani 12, na Posho ya miezi 36 ya kujiandaa na makazi mapya.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.