• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

STANBIC YAPONGEZWA KWA MSAADA WA VIFAA TIBA MWANZA

Posted on: November 27th, 2025

Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana ameupongeza na kuushukuru uongozi wa benki ya stanbic kwa kuchangia vifaa tiba vyenye thamani ya zaidi ya shilingi Milioni 19 ambavyo vitaenda kuwa na mchango mkubwa katika hospitali na kuboresha huduma za afya.

Amesema hayo leo Novemba 27, 2025 wakati akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mwanza katika hafla ya kukabidhiana vifaa tiba ambavyo ni viti mwendo 10, vitanda na magodoro yake 10 pamoja na mashuka 200 kwa hospitali za Wilaya za Nyamagana na Ilemela iliyoandaliwa na benki ya Stanbic katika viwanja vya ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Bw. Balandya amesema kuwa serikali imeendelea kufanya jitihada za kupambana na adui wa maendeleo ambae ni maradhi na kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya na kuwawezesha kushiriki kikamilifu katika shudhuli za ujenzi wa taifa kwakua sekta ya afya ni sekta muhimu sana kwa maendeleo ya wananchi.

“Sekta ya afya ni sekta muhimu sana kwa maendeleo ya wananchi popote pale duniani na kwa kutambua hili hata Baba wa Taifa letu Mwalimu Julius Nyerere wakati akitaja maadui wa taifa letu alijumuisha suala la afya”. Amesema Bw. Balandya.

Sambamba na hayo amewasihi wananchi kuendelea kujitokeza hospitali na vituo vya kutolea huduma za afya kwa wakati ili waweze kujua hali ya miili yao kwa kupima na kupata huduma za matibabu kwa wakati.

Naye Meneja wa benki Stanbic tawi la Mwanza Bw. Geoffrey Makondo amesema utoaji wa huduma bora kwa jamii ni kwa kuanza kutoa misaada kwa jamii husika na wao wamechagua kuigusa jamii ambayo wanafanya nayo kazi kila siku kwa kuichangia katika sekta ya afya.

Ameongeza kuwa katika kutimiza miaka 30 ya kihudumia jamii benki itaendelea kushirikiana vyema na serikali pamoja na watumishi wake ili kuhakikisha wanaendelea kukuza shughuli za kiuchumi na maendeleo katika taifa.

Akimuwakilisha Mganga Mkuu Mkoa wa Mwanza, Dkt. Kwandu Mashuda ameishukuru benki ya Stanbic kwa kuikumbuka idara ya afya kwakua ni idara nyeti na yenye uhitaji mkubwa na amesema wataenda kuvitumia vyema vifaa hivo na kuleta tija kwa wagonjwa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • STANBIC YAPONGEZWA KWA MSAADA WA VIFAA TIBA MWANZA

    November 27, 2025
  • RC MTANDA AWATAKA TAPHATA KUHAKIKISHA WANATOA ELIMU SAHIHI YA MATUMIZI YA DAWA

    November 26, 2025
  • RC MTANDA AIPONGEZA OFISI YA WAZIRI MKUU KUANZISHA KAMATI ZA MAAFA ZA MIKOA

    November 18, 2025
  • RC MTANDA AWATAKA WATAKWIMU KUTOA TAKWIMU SAHIHI KUCHAGIZA MAENDELEO

    November 18, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.