• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

TCRA Yawaonya matapeli wa Mitandao

Posted on: June 13th, 2019

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema kuanzia Januari Mosi, 2020  kila mtu atatakiwa kumiliki laini moja ya kampuni moja ya simu ya mkononi.

Kauli hiyo imetolewa na Meneja wa TCRA kanda ya Ziwa, Mhandisi Francis Mihayo katika mkutano  wa wadau wa sekta ya mawasiliano  uliolenga kupokea kero na mapendekezo juu ya utendaji wa mamlaka hiyo.

Mkutano huo ulishirikisha viongozi wa dini mbalimbali,wamiliki wa vituo vya redio, mitandao ya kijami na mafundi simu ambapo wengi wao waliomba TCRA kushirikiana na  Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) ili kuweza kupata vitambulisho kwa wakati.

Mhandisi Mihayo alisema kwa mtu atakaye hitaji kuwa  na laini mbili atatakiwa kuandika maelezo ya uhitaji huo.

Alisema, imelazimika kuunda kundi maalum ‘group’ linaloshirikisha watoa huduma za mawasiliano  nchini kwa ajili ya kuziharibu simu za matapeli  wanaotuma ujumbe mfupi wa maneno (sms) kwa watu ili kujipatia fedha  kwa njia zisizo rasmi.

Pia imewaonya watu maarufu  wakiwamo wanasiasa wanatumia mitandao ya kijamii  kusambaza taarifa ambazo zinapotosha jamii kuhusu jambo lolote na kuwataka kuacha mamlaka husika au vyombo vya habari kusema kwa kuzingatia maadili ya kazi zao.

“Moja ya malalamiko sugu katika suala la mawasiliano ni watu kutumia ujumbe wa utepeli, kweli watu wametapeliwa sana, wapo wanaolalamika kupata ujumbe usiku na kusababisha  mgogoro katika ndoa lakini kama TCRA na watoa huduma tukaamua kuunda group letu la kuwashughulikia watu wa namna hiyo”alisema

Mhandisi Mihayo alisema TCRA  imeendelea kutoa elimu kwa jamii ikiwa ni pamoja na kufanya mikutano, kuchapisha majarida, vyombo vya habari lengo likiwa ni kujua namna ya kutumia sekta ya mawasiliano kwa faida na kuziomba taasisi za dini  kuelimisha waumini wao.

Alisema  mmomonyoko wa maadili  katika familia umetokana na wazazi kuwaruhusu  watoto wadogo kutumia simu za mikononi jambo ambalo linawafanya kuangalia picha za ajabu.

Mhandisi Mihayo alisema, baadhi ya watu maarufu wamekuwa wakitumia mitandao ya kijamii kuandika mambo yasiyo ya kweli  huku jamii  ikiwaamini kuliko vyombo vya habari vyenye leseni na kuwataka kuwa makini na taarifa wanazoweka mitandaoni kwani wanawafuatilia kwa ukaribu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.