• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

TEMESA watakiwa kuboresha huduma ili kujenga imani kwa wateja wao

Posted on: May 24th, 2023

**TEMESA watakiwa kuboresha huduma ili kujenga imani kwa wateja wao*


Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) wametakiwa kubadilika na kuboresha huduma zao kwa wateja ili kuwa mfano wa utoaji wa huduma bora.

Akifungua Warsha ya Wadau wa TEMESA leo kwa niaba ya Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza, Katibu Tawala Msaidizi Mipango na Uratibu Ndg.Joachim Otaru amesema kwa muda mrefu Taasisi hiyo imekuwa ikilalamikiwa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo huduma duni, kutokuwa waaminifu wa vipuri,na ucheleweshaji wa matengenezo ya magari.

Otaru amebainisha baada ya Serikali ya awamu ya Sita kuanza kuiboresha Taasisi hiyo kuanzia ngazi ya uongozi, fedha na vifaa,sasa ni jukumu la TEMESA kutoa huduma zenye tija.

" Kabla sijaingia kufungua Warsha hii nimeoneshwa hapo aina ya huduma mnazotoa kwenye magari na mitambo mkiwa na vifaa vya kisasa pamoja na gari maalum la utoaji wa huduma na nimeambiwa vifaa hivyo vipo nchi nzima,hongereni sasa onesheni ubora wenu," amesema Otaru.

Ameongeza kuwa wateja wote wanaodaiwa na TEMESA wafanye hima kulipa madeni yote ambapo Mkoa wa Mwanza una wadai wateja wake deni la zaidi ya Shs Bilioni 1.45,fedha ambazo ni nyingi zinazochongia kurudisha nyuma utoaji wa huduma.

"Tumezifanyia kazi changomoto nyingi zilizokuwa zinatukabili ambapo Mafundi wetu wanaendelea kupatiwa mafunzo kwenye vyuo mbalimbali,Karakana zetu zote 13 nchini tumefunga camera za kisasa za kubaini aina yoyote ya wizi wa vipuri,kwa kifupi utoaji wa huduma zetu umekuwa wa kiwango kizuri tofauti na hapo awali," Mhandisi Hussein Karonda,Kaimu Mtendaji Mkuu,TEMESA.

"Kituo chetu cha Mwanza licha ya kuwadai wateja wetu fedha nyingi lakini tunashukuru Serikali imezidi kutuwezesha kila mwaka,mfano mzuri ni vifaa hivi na gari maalum lenye gharama ya Shs Milioni 700 vinavyotupa ari ya utoaji wa huduma bora kwa magari na mitambo ya Serikali," Mhandisi Gilly Gabriel Chacha,Meneja wa TEMESA Mwanza.

Aidha baadhi ya Wadau wa Taasisi hiyo wamepatiwa hati maalum kutokana na kutambua mchango wao akiwemo aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Adam Malima na baadhi ya Wazabuni wa Vipuri wanaoendelea kushirikiana na TEMESA kutoa huduma kwa wateja.

Warsha hiyo yenye lengo la kuwasikiliza Wadau kuhusiana na changamoto zilizopo na kuzipatia ufumbuzi imewashirikisha Makatibu Tawala wa Wilaya zote za Mwanza,Mameneja wa Mikoa wa TEMESA,Wakurugenzi wa Halmashauri za Mwanza pamoja na Wazabuni wa Vipuri.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.