• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

TFDA Yatoa mafunzo kwa wanahabari Mkoa wa Mwanza na Shinyanga

Posted on: May 22nd, 2018


Imeelezwa kuwa afya ya watumiaji bidhaa mbalimbali zitalindwa na kuboreshwa ikiwa sheria ya Chakula, Dawa na Vipodozi sura 219, itasimamiwa na kutekelezwa ipasavyo huku vyombo vya habari vikitimiza wajibu wao kwa usahihi.

Hayo yalisemwa na Mkurugenzi Msaidizi wa Habari Maelezo Zamaradi Kawawa katika kikao kazi cha Wahariri na Waandishi wa Habari kutoka mikoa ya Mwanza na Shinyanga kuhusu uhamasishaji wa sheria ya Chakula,Dawa na Vipodozi sura 219 kilichoandaliwa na Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) kilichofanyika mkoani hapa.

Kawawa alisema, wahariri na waandishi wa habari wanamchango mkubwa katika kuhimiza utekelezaji wa sheria hiyo,kuelimisha umma kwa kuwapatia taarifa sahihi zinazohusu shughuli za udhibiti wa bidhaa hizo kutoka vyanzo mbalimbali sambamba na kuijua sheria hiyo.

Alisema, vyombo hivyo vinawajibu wa kutumia kalamu zao kuleta mabadiliko chanya katika jamii kuhusu udhibiti wa bidhaa,kuielimisha juu ya kuzingatia ubora na usalama wa bidhaa hizo pamoja na kuwaibua watu wanaovunja sheria hiyo kwa kutoa taarifa TFDA na kwa vyombo vingine vya sheria vinavyohusika na udhibiti.

“Wana habari waendelee kutoa elimu kwa jamii juu ya madhara watakayo yapata kiafya endapo watatumia bidhaa za chakula,dawa,vipodozi,vifaa tiba na vitendanishi ambayo vipo kinyume na sheria sambamba na kutoa mapendekezo kwa TFDA juu ya namna ya kuboresha usimamizi na utekelezaji wa sheria,”alisema Zamaradi.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mkuu TFDA Agnes Kijo alisema,suala la afya ni la jamii nzima,hivyo ni wajibu wakila mtu katika kudhibiti bidhaa bandia na duni,huku waandishi wakiendeleza ushirikiano na mamlaka hiyo katika kuibua wafanyabiashara ambao siyo waaminifu wanaouza bidhaa zilizopita muda.

Kijo alisema, kwa mwaka wanatumia zaidi ya milioni 100 katika kufanya opareshini na ukaguzi maalum wa kudhibiti bidhaa hizo,hivyo ni vyema wananchi wakahamasishwa na kuelimishwa kuacha kutumia ili fedha hizo zitumike kwenye miradi ya maendeleo.

Naye Mwanasheria Mshauri wa TFDA Iskari Fute alisema,madhumuni ya sheria ni kuweka mfumo thabiti wa usalama,ubora na ufanisi wa chakula,dawa,vipodozi,vifaa tiba, vitendanishi,vifaa vya maabara na dawa zenye asili ya miti shamba pamoja na kulinda afya ya jamii ili kutekeleza msingi wa haki ya kuishi.

Hata hivyo Mkurugenzi wa Dawa na Bidhaa Nyongeza wa TFDA Adam Fimbo alisema, bidhaa wanazodhibiti ni zile zenye athari moja kwa moja katika afya ya binadamu,hivyo waandishi wa habari wanamchango mkubwa wa kuelimisha jamii kuhusu matumizi sahihi ya bidhaa hizo.

Aidhaa baadhi ya washiriki wa kikao hicho,waliitaka mamlaka hiyo kufika hadi maeneo ya vijijini kutoa elimu kuhusu madhara yatokanayo na utumiaji wa vipodozi vyenye viambato vyenye sumu na bidhaa bandia na duni.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. July 29, 2022
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2022 July 03, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI ICAP October 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC Malima awataka Madiwani kusimamia na kuendeleza vyema rasilimali za Bonde la Ziwa Victoria

    March 31, 2023
  • RC Malima awahimiza Wana Mwanza kufurika Dimbani Nyamagana Jumamosi hii kuwashangilia wana TP LINDANDA Pamba FC dhidi ya Kitayose

    March 30, 2023
  • Makinda awataka wasomi na wananchi kuyatumia matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi kujiinua kiuchumi

    March 29, 2023
  • RC Malima ahimiza kutokomeza unyanyasaji wa kijinsia

    March 27, 2023
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 33180, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras.mwanza@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.