• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

TUENDELEE KUMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUTANUA WIGO WA AJIRA NCHINI: RC MTANDA

Posted on: May 1st, 2024

TUENDELEE KUMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUTANUA WIGO WA AJIRA NCHINI: RC MTANDA


Mkoa wa Mwanza leo umesheherekea Sikukuu ya Wafanyajazi, Mei Mosi  kwa kumshukuru Rais Samia kwa kuendelea kutanua wigo wa ajira kutokana na  ujenzi wa miundombinu mbalimbali hapa nchini.

Akizungumza na wafanyajazi kwenye uwanja wa CCM Kirumba, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Said Mtanda amesema miradi mingi inayofanyika mkoani humo imetoa nafasi za ajira pamoja na kuwatengenezea vijana mazingira mazuri ya kujiajiri.

"Mradi kama wa Daraja la JP Magufuli umetengeneza ajira 1875, hali ambayo imesaidia kuongezeka vipato kwa familia na kupunguza idadi ya vijana  kukaa vijiweni kutokana na kukosa kazi",amesema Mkuu huyo wa Mkoa.

Amesema Serikali ya awamu ya Sita imekuwa na sikio kwa Shirikisho la Wafanyajazi TUCTA kwa kuongeza mishahara huku ikitenga bajeti kwa ajili ya kuwatengenezea vijana mazingira ya kujiajiri.

Akizungumzia kauli mbiu ya mwaka huu isemayo nyongeza ya mishahara ni msingi wa mafao bora na Kinga dhidi ya hali ngumu za maisha,Mtanda amebainisha ni sahihi wafanyajazi kuwa na maslahi bora lakini siku zote mshahara huwa hautoshi.

"Natoa rai kwa wafanyajazi wenzangu tujenge utamaduni wa kubuni vyanzo vya mapato halali kama ni kilimo au ufugaji,hii itasaidia kuongeza vipato kwenye familia zetu",Mkuu wa Mkoa.

Mratibu wa Sherehe za Mei Mosi Mkoani Mwanza Halfan Nyungwa amebainisha bado baadhi ya Taasisi binafsi zimekuwa Waziri kuwasilisha michango ya Wafanyajazi hali ambayo inaleta usumbufu na mlomlongo wa kesi za madai kwenye tume zinazoshughulika na migogoro ya Wafanyajazi.

"Tunaiomba Serikali iangalie upya Sheria kwenye mifuko ya Jamii,bado inaonesha haina nguvu ya kutosha kushughulika na Taasisi zinazozembea kuwasilisha michango ya Wafanyajazi",Mratibu wa Sherehe.

Sherehe hizo zilizofanyika Ki-mkoa Wilayani Ilemela,zimekwenda pamoja na kukabidhiwa zawadi kwa baadhi ya Wafanyajazi bora.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.