• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

TUENDELEE KUSHIKAMANA WANA MWANZA PAMBA JIJI FC ITIMIZE LENGO LA KUCHEZA LIGI KUU MSIMU UJAO-RC MAKALLA

Posted on: September 15th, 2023

TUENDELEE KUSHIKAMANA WANA MWANZA PAMBA JIJI FC ITIMIZE LENGO LA KUCHEZA LIGI KUU MSIMU UJAO-RC MAKALLA


*Asema siri ya kufikia malengo ni mshikamano wa pamoja kutoka kwa mashabiki


*Aonesha matumaini ya kucheza Ligi kuu kutokana na ubora wa Pamba Jiji FC


Wakati wana TP Lindanda wakiendelea kung'ara kwa mfululizo wa ushindi michuano ya soka  Ligi ya Championship kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Pan African,Mkuu wa Mkoa wa Mwanza CPA Amos Makalla ameendelea kuwaomba mashabiki wa soka kuendelea kuipa ari timu hiyo kwa kufurika uwanjani katika kila michezo ya timu hiyo.

Mkuu huyo wa Mkoa ambaye pia ni mlezi wa timu biyo akizungumza na vyombo vya habari leo kwenye uwanja wa Nyamagana mara baada ya mpambano,amesema huu ni mwanzo mzuri ambao unaleta matumaini ya kucheza Ligi kuu msimu ujao.

"Siku zote shabiki uwanjani ni mchezaji wa 12  hivyo napenda kuwaomba tuendelee kushikamana kwa pamoja kwa lengo la kuwatia moyo wachezaji wetu wazidi kufanya vizuri,"Mhe.Makalla

Mhe.Makalla amebainisha Ligi ya Championship ni ngumu kutokana na timu zinazopambana kupanda Ligi kuu ni nyingi na zenye uwezo,hivyo wajibu wa kila mwana Mwanza ni kuwaunga mkono wana TP Lindanda.

Katika mchezo huo Pamba Jiji FC walilazimika kupata ushindi huo muda wa lala salama kwa mkwaju wa penati uliofungwa na mchezaji Jamal Mtegeta na kuamsha shamra shamra na nderemo kutoka kwa mashabiki waliofurika uwanjani hapo.

Mara baada ya filimbi ya mwisho kuashiria kuhitimisha mpambano huo,mlezi wa timu hiyo akiongozona na Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe.Amina Makilagi,Mbunge wa Jimbo la Nyamagana,Mhe.Stanslaus Mabula na Meya wa Jiji Mhe.Sima Costantine Sima walishuka uwanjani na kuwapongeza Pamba Jiji FC kwa ushindi huo.

Wana TP Lindanda msimu huu wakiwa na mchanganyiko mzuri wa wachezaji waliotamba Ligi kuu msimu uliopita,mchezo wa fungua dimba uliopigwa uwanja wa Nyamagana waliichakaza timu ya Cosmo Politan kutoka Da- re-Salaam kwa mabao 4-0 kabla ya leo kuwafunga Pan African bao 1-0

Baada ya michezo hiyo miwili ya nyumbani ya Ligi ya Championship,Pamba Jiji FC sasa mchezo ujao watasafiri hadi Shinyanga kuumana na Stendi Utd Ijumaa ijayo kwenye dimba la Kambarage.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.