• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Tumieni Jukwaa hili la mkutano wenu mkuu ili mje na maboresho zaidi katika sekta ya elimu nchini: Naibu Waziri Ndejembi

Posted on: December 15th, 2023

Tumieni Jukwaa hili la mkutano wenu mkuu ili mje na maboresho zaidi katika sekta ya elimu nchini: Naibu Waziri Ndejembi


Naibu Waziri wa nchi Ofisi ya Rais,Tamisemi Mhe. Deogratius Ndejembi ameutaka umoja wa walimu wa shule za Sekondari nchini TAHOSSA kuutumia mkutano wao mkuu wa 18 unaofanyika Mkoani Mwanza kama jukwaa la kuleta mageuzi chanya katika sekta ya elimu nchini.

Mh.Ndejembi ametoa rai hiyo leo wakati akifungua mkutano huo kwenye ukumbi wa Malaika Beach Resort, amebainisha umoja huo ni chombo muhimu katika kuleta maendeleo hivyo yote yatakayojadiliwa kwenye mkutano huo yawe na tija kwa Taifa letu.

"Rais wetu ameonesha nia ya dhati ya kupigania maendeleo ya nchi yetu kwa kuboresha sekta ya elimu, wote ni mashuhuda wa fedha za Uvico19 zilivyo jenga madarasa bora nchini nzima, ni wajibu wetu sisi kumuunga mkono kwa vitendo ili kutimiza ndoto yake ya kuona Taifa linazidi kustawi kwa viwango bora vya elimu kwa wanafunzi," Naibu Waziri.

Amewahimiza wakuu hao wa shule kuendelea kuwa wafanyakazi wa mfano kama walivyoonesha wakati wa ujenzi wa madarasa yaliyokamilika kwa wakati, ubora unaokwenda na thamani ya fedha na weledi wa matumizi ya fedha zilizo kusudiwa.

Aidha katika Mkutano huo Mhe. Ndejembi alitoa maamuzi ya kiwanja cha TAHOSSA kilichopo eneo la Ihumwa, Dodoma kilicholengwa kama kitega uchumi chao, warejeshewe mara moja baada ya kupewa taasisi ya MKURABITA ambayo tayari imefutwa, alipompigia simu ya hadharani Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma na kumpa maelekezo hayo.

Awali akimkaribisha mgeni rasmi wa mkutano huo Katibu Tawala wa mkoa wa Mwanza,Ndg.Balandya Elikana amesema mwaka  2023-24 wamepokea jumla ya Shs bilioni 89.7 kwa ajili ya kuboresha miundombinu katika sekta ya elimu hali iliyochangia kuwa na madarasa bora na wanafunzi kusomea katika mazingira rafiki yasiyo na msongamano.

"Ndugu Naibu Waziri Ofisi ya mkuu wa mkoa imesimama imara kuhakikisha miradi yote iliyokusudiwa katika sekta ya elimu inakamilika kwa wakati na kwa ubora unaokwenda na thamani ya fedha,"amesema mtendaji huyo wa mkoa mbele ya wakuu wa shule za sekondari.

Rais wa TAHOSSA Dennis Otieno amesema katika siku tatu za mkutano wao watajadili mambo mbalimbali ya kuboresha elimu nchini ikiwemo kuzitambua na kuzipa zawadi maalum shule zinazofanya vizuri na zile zisizofanya vizuri kuona zinakabiliwa na changamoto gani ili kupata ufumbuzi.

Mkutano huo unatarajiwa kufungwa Disemba 17,2023 na Waziri wa nchi Ofisi ya Rais,Tamisemi Mhe.Mohamed Mchengerwa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.