• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

UIMARISHWAJI WA MIFUMO YA KIELETRONIKI IMEONGEZA UWAJIBIKAJI – RAS BALANDYA

Posted on: July 23rd, 2025

Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Ndugu Balandya Elikana amesema uimarishwaji wa matumizi ya mifumo ya Kielektroniki imekuwa na manufaa makubwa, imeongeza tija na uwajibikaji katika utendaji wa shughuli za Serikali na taasisi zake, pamoja na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Katibu Tawala ameyasema hayo leo Julai 23, 2025 wakati akifungua mafunzo ya matumizi ya mfumo wa kielektroniki wa taarifa za utekelezaji wa programu za maboresho nchini yaliyofanyika jijiji Mwanza na kujumuisha Mikoa mitatu ya Mwanza, Shinyanga na Geita.


Aidha, Katibu Tawala amesema mifumo imepunguza gharama na kuongeza upatikanaji wa taarif na kwa msingi huo, ili kurahisisha uwasilishaji wa Taarifa za Utekelezaji wa Mkakati, Serikali imeandaa mfumo wa taarifa za utekelezaji wa programu za maboresho nchini ukiwemo mkakati wa Taifa dhidi ya rushwa awamu ya nne.

“Serikali ingependa kuona kuwa rushwa inatokomezwa katika utoaji huduma ili kuiwezesha kutekeleza ipasavyo jukumu lake la Kikatiba la uwepo wa Ustawi wa Wananchi kama lilivyotamkwa kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977, Ibara ya 8 (1) (b).)”.


Sambamba na hayo Bw. Balandya amesema ni wajibu wa kila taasisi kuhakikisha kuwa utekelezaji wa mkakati wa Taifa dhidi ya rushwa awamu ya nne unasimamiwa na taarifa za utekelezaji zinawasilishwa kwa Katibu Mkuu Kiongozi kwa wakati.

“Hivyo, mafunzo ya matumizi ya mfumo huu ambayo yatachukua siku mbili ni ya msingi kwetu sote katika kuhakikisha kuwa taarifa husika zinachakatwa na kuwasilishwa kwa wakati”.


Ndugu Balandya ameishukuru Ofisi ya Rais, Ikulu kwa kuona umuhimu wa kutoa mafunzo hayo kwa mikoa ya Mwanza, Shinyanga na Geita na amewasisitizia washiriki kwamba, baada ya mafunzo hayo wautumie kikamilifu mfumo huo kuchakata na kuwasilisha taarifa za utekelezaji kwa wakati.

Tukumbuke kuwa taarifa za utekelezaji wa mipango kazi zina mchango katika maamuzi mbalimbali ya msingi ya kitaifa. Hivyo suala hili tulipe umuhimu wake ili matokeo tarajiwa ya utekelezaji wa Mkakati wa Taifa dhidi ya rushwa yaweze kufikiwa. Ameongeza Katibu Tawala.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WAKULIMA WAASWA KUTUMIA TEKNOLOJIA KUFANYA KILIMO CHA KISASA

    August 02, 2025
  • RMO MWANZA AONGOZA ZIARA YA MAFUNZO YA USAFI NA MAZINGIRA MKOANI IRINGA

    July 21, 2025
  • RAS BALANDYA ATOA MAAGIZO UTEKELEZAJI WA MIRADI SENGEREMA

    July 30, 2025
  • UIMARISHWAJI WA MIFUMO YA KIELETRONIKI IMEONGEZA UWAJIBIKAJI – RAS BALANDYA

    July 23, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.