• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Ukerewe Yawezeshwa Vifaa Tiba

Posted on: April 8th, 2019


Hospitali ya Uhuru  imetoa msaada wa hadubini mbili ‘microscope’ zenye thamani ya  Sh milioni 6 kwa Wilaya ya Ukerewe mkoani Mwanza kutokana na uwepo wa mahitaji makubwa ya vifaa tiba hasa za uchunguzi.

Akikabidhi  mashine hizo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji  wa Taasisi ya Uhuru, Dkt. Derrick Nyasebwa, Mkurugenzi wa Tiba na bingwa wa upasuaji, Dkt. Emmanuel  Kanumba alisema  kama taasisi imefikia hatua ya kuisaidia Wilaya ya Ukerewe kutokana na ombi lao.

Dkt. Kanumba alisema  mazingira ya wilaya ya Ukerewe  yalivyo inapaswa kusaidiwa katika sekta ya afya kwani  bila wananchi wa kisiwa hicho kuwa na afya njema hakuna maendeleo yatakayopatikana.

“Taasisi ya Uhuru hosptali  inashirikiana na serikali na wadau mbalimbali kuhakikisha suala la afya halibaki kuwa jukumu la watu fulani bali ni   la wote hivyo  tumetoa msaada wa microscope  baada ya kubaini upungufu huo uliopo katika wilaya ya Ukerewe.

Mara zote tumekuwa tukishiriki katika vikao mbalimbali vya sekta ya afya lakini  taarifa nyingi kutoka Ukerewe ni upungufu wa vitendea kazi, sasa tukaona ni heri tukasaidia hizi mashine na imani yetu masuala ya vipimo vya maradhi  hayatakuwa na shida tena,”alisema Dkt. Kanumba.

Dkt. Kanumba alisema hivi karibuni Serikali imezindua kampeni ya  uwajibikaji katika kuzuia vifo vitokanavyo na uzazi iliyokuwa na kauli mbiu ya ‘Jiongeze Tuwavushe salama’ hivyo  kama taasisi ya  Uhuru imeshiriki vema kwa kutoa mashine hizo ambazo zitakwenda kupima maradhi ya wagonjwa watakaofika  hospitalini kupata tiba.

Alisema wamekuwa na utaratibu wa kusaidi jamii pale inapohitajika ambapo aliongeza kwamba hata watoto yatima hutibiwa bure na wale wenye kipato duni hutibiwa kwa gharama nafuu.

Aliwataka jamii kutoogopa kwenda hospitali za binafsi kwani kwa kuogopa gharama bali huwa zinasikiliza  maombi ya mgonjwa na kumtibu kwa gharama nafuu.

Akipokea msaada huo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe, Lucas Magembe, Mkuu wa Wilaya ya Sengerema, Emmanuel Kipole, alishukuru uongozi wa hospitali hiyo kuona umuhimu wa kuisaidia jamii.


Kipole alisema vifaa hivyo vitakwenda kuitumiaka kama ilivyokusudia  na kuwataka watumishi ndani ya wilaya hiyo kuituna mashine hiyo ili iweze kuwasaidia wananchi wengi.

Hivi karibuni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe.John Mongella aliwasainisha  kiapo  cha uwajibikaji wakuu wa wilaya zote za mkoa huo  juu ya kupunguza vifo vya wajawazito na watoto wachanga ambapo aliwataka kila mmoja awajibike katika eneo lake na  kutoa taarifa ya utekelezaji kila baada ya miezi mitatu.

Tukio hilo lilifanyika wakati wa uzinduzi wa kampeni ya uwajibikaji katika kuzuia vifo vitokanavyo na uzazi iliyokuwa na kauli mbiu ya ‘Jiongeze Tuwavushe salama’   ambapo Mhe.Mongella alisema takwimu zinaonyesha kwamba mwaka 2017 jumla ya wanawake 195 walipoteza maisha kutokana na uzazi huo.

Mongella alisema kutokana na jitihada za Serikali za kupunguza haali hiyo, mwaka 2018 vifo hivyo vimepungua na kufikia 151 lakini kuanzia Januari mwaka huu tayari vifo 46  vitokanavyo na uzazi vimetokea ndani ya mkoa huo.






Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.