• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

UKITAKA KUIPENDA KAZI YAKO IKUBALI KWANZA - RC MTANDA

Posted on: July 29th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewaasa Maafisa Tarafa na Watendaji wa Kata kuweka jitihada kwenye kazi zao kwa kuzikubali nafasi zao na kutekeleza majukumu yao kwa bidii ili waweze kuleta tija katika jamii wanazoziongoza.


Mhe. Mtanda ameyasema hayo leo tarehe 29 julai, 2025 wakati akiwahutubia Watendaji na Maafisa hao zaidi ya 300 kutoka katika Mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Mara, Simiyu, Geita, Tabora na Kagera walioajiriwa

Kuanzia Julai, 2024.

“Kazi yako ukiipenda utaifanyia juhudi, na ukifanikiwa hayo basi utajikuta umejiendeleza kielimu, kuweka weledi na nidhamu, kwa ujumla kuishi ndani ya utumishi huo kizalendo.” Mhe. Mtanda.

Aidha, amewataka kutumia taaluma zao kuonesha tabia njema kwa jamii inayowazunguka na kuonesha uwezo kwenye kazi zao na staha ya maisha kwenye maeneo yao ya uongozi.

Kadhalika, amewataka kwenda kufanya maamuzi sahihi yanayozingatia sheria, kanunu na miongozo iliyowekwa katika sekta husika mathalani ardhi na sio kufanya uonevu kwa kundi moja au jingine kwani hali hiyo uharibu kazi.


Vilevile Mkuu wa Mkoa amewataka kwenda kuwaunganisha wananchi na sio kuwagawanya pia kuhakikisha wanawajengea ari ya kujitolea kwa serikali yao hususani kwenye uanzishwaji wa miradi ya maendeleo kama ujenzi wa madarasa, miradi ya maji na barabara.

Hata hivyo, amewataka kuishi kuendana na mazingira watakayoyakuta kwa wananchi wanaoishi nao katika maeneo yao ya kazi na kuwa wabunifu mathalani waonapo vyanzo vya mapato vipya na kuviwasilisha kwenye Halmashauri ili vipitiwe na kuingizwa katika maoteo ya kodi na ushuru.


Katika mafunzo hayo washiriki wamejengewa uelewa wa kina kuhusu muundo na majukumu yao ya kikazi, sera na sheria za Serikali, mbinu za kusimamia miradi ya maendeleo, namna ya kushughulikia kero za wananchi kwa wakati, pamoja na usimamizi bora wa rasilimali na mapato ya ndani.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANAHABARI, JESHI LA POLISI WAASWA KULINDA AMANI KIPINDI CHA UCHAGUZI

    August 07, 2025
  • RAS GEITA AWAALIKA WANANCHI KUJIFUNZA KILIMO CHA KISASA NANE NANE NYAMHONGOLO

    August 07, 2025
  • RAS GEITA AWAALIKA WANANCHI KUJIFUNZA KILIMO CHA KISASA NANE NANE NYAMHONGOLO

    August 07, 2025
  • WALIOBEBA MAFANIKIO YA MKOA KITAALUMA WAPONGEZWA

    August 06, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.