• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Upimaji wa Virusi vya UKIMWI waongezeka Mwanza

Posted on: December 1st, 2018

Upimaji wa Virusi vya UKIMWI waongezeka Mkoani Mwanza.Hayo yamebainishwa leo katika Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani ambayo yamefanyika Kimkoa katika Viwanja vya Furahisha wilaya ya Ilemela.

Akiongea kwenye Maadhimisho hayo Mgeni rasmi Mhe. Dkt Severin Lalika amesema Upimaji wa VVU umeongezeka Zaidi katika Mkoa wetu kupitia kampeni iliyozinduliwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza tarehe 21/07/2018 katika viwanja vya furahisha ambapo kwa siku hiyo peke yake watu 2006 walipimwa wanaume wakiwa 1,234 na wanawake wakiwa 772 na jumla ya watu 167 waligundulika kuwa na maambukizi ya VVU,wanaume 94 na wanawake 73

Aidha Halmashauri ziliendelea na Kampeni hiyo ya upimaji na kufanya jumla ya watu 714,842 kupima afya zao ,wanaume 252,539 na wanawake 462,303 ambapo kwa Idadi hiyo watu 8,197 waligundulika kuwa na maambukizi ya Virusi vya UKIMWI

Mhe.Dkt Severin amesema kutokana na Takwimu zilizopo zinazoonesha Maambukizi ya UKIMWI Mkoani Mwanza zimepanda kutoka Asilimia 4.2 mpaka Asilimia 7.2 kwa Mwaka 2016/17  hivyo kuwataka wananchi pamoja na wadau mbalimbali kuendelea kuunga mkono Jitihada zinazofanywa na wananchi pamoja na wadau mbali mbali za kupunguza maambukizi ya Virusi vya UKIMWI

Akitoa Salamu za Nyamagana Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Dkt.Phillis Nyimbi amesema kutokana na takwimu za maambukizi ya Virusi vya UKIMWI,Nyamagana imeonekana inaongoza kuwa na Idadi Kubwa ya maambukizi  ambapo watu 23,583 wamegundulika kuwa na Virusi vya UKIMWI“Mimi kama msimazi mkuu wa wilaya ninalichukua hili na kwenda kuwashirikisha viongozi wengine wilayani kwangu na kulifanyia kazi”  amesema Dkt Nyimbi

Aidha Dkt Nyimbi amewataka wadau mbali mbali wanaojishughulisha na shughuli za Afya kufika Ofisini kwake nayeye yupo tayari kutoa ushirikiano kupunguza kiwango hicho cha maambukizi

Akisoma Taarifa ya Maambukizi ya UKIMWI kimkoa Mratibu wa UKIMWI Mkoa Dkt Pius Masele amesema kwa Takwimu za Mwaka 2017 /18, Mwanza umekua Mkoa wa Nne kitaifa kuwa na Idadi kubwa ya maambukizi ya Virusi vya UKIMWI ambapo kiwilaya Nyamagana ikishika nafasi ya Kwanza kuwa na Idadi ya watu 23,583 walioambukizwa VVU



Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.