• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Uzinduzi wa ugawaji vyandarua bure kwa wanafunzi wafanyika Mwanza

Posted on: October 10th, 2019


Zoezi la ugawaji  vyandarua bure kwa wanafunzi wa shule za msingi Mkoani Mwanza limezinduliwa rasmi oktoba 10 mwaka huu ambapo jumla ya vyandarua 445,254 vinategemea kugawiwa.

Akifungua zoezi hilo wakati wa hafla fupi iliyofanyika katika shule ya msingi Nyanza mkoani hapa, Mkuu wa Mkoa Mhe.John Mongella amesema kuwa ugawaji wa  vyandarua hivi ni ishara ya kuendelea kwa mapambano dhidi ya ugonjwa wa malaria.

"Kama mnavyojua Ugonjwa wa malaria bado umeendelea kuwa tishio kwa kina mama na watoto na hata wanume pia, leo tupo hapa kuanza rasmi ugawaji wa vyandarua kwa wanafunzi wa shule za msingi mkoani kwetu.

"Tumeamua kuanza na watoto wa shule za msingi kwa sababu hawa ndiyo watu wazima wa kesho hivyo tukiwajengea utamaduni wa matumizi sahihi ya vyandarua itajengeka kuwa tabia yao  kumbe wataendeleza hata watakapokuwa na maisha yao ya kujitegemea.

"Mpaka sasa takwimu zinaonyesha kuwa maambukizi ya malaria kitaifa yameshuka hadi asilimia saba huku sisi kama Mkoa tuna asilimia nane na hii inaonyesha wastani wetu upo juu zaidi ya wastani wa taifa.

"Hivyo niwaombe tuendelee kushirikiana sote kwa pamoja ili baada ya miaka kadhaa ijayo tuwe tumefikia asilimia sifuri na nina amini inawezekana kama kila mmoja atakubali kuweka nguvu zake kuhakikisha tunatokomeza ugonjwa huu,"alisema Mongella.

 "Niwaagize viongozi wote kuanzia ngazi ya Mkoa hadi ngazi ya shule kuhakikisha zoezi hili linasimamiwa kikamilifu ili vyandarua hivi viweze kugawiwa kwa madarasa yaliyokusudiwa bila upendeleo na mwisho wa siku kuwe na matokeo chanya katika kutokomeza malaria,"alisema Mongella.

Awali akisoma taarifa fupi juu ya mwenendo na matarajio ya zoezi hilo Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa, Tuloson Nyalanja alisema kuwa mpango wa ugawaji vyandarua hivi ni endelevu na unategemewa kuwa chachu ya kuzima ugonjwa wa malaria Mkoa wa Mwanza na Tanzania kwa ujumla.

"Zoezi hili mwaka huu linafanyika kwa awamu ya nne mfululizo ambapo lilianza rasmi  mwaka 2016 na mpaka sasa limekuwa na manufaa ingawa bado kuna changamoto ya matumizi sahihi ya vyandarua.

"Kama ilivyo kawaida yetu tumelenga kuzifikia shule zote 976 mfululizo zilizopo kwenye halmashauri nane za Mkoa wa Mwanza ambapo tutawagawia vyandarua wanafunzi wote wa darasa la tatu hadi la sita kwa muda wa wiki mbili.

"Mbali na kugawa vyandarua lakini kwa Mwaka huu tumewekeza nguvu zaidi kutoa elimu ya matumizi sahihi ya vyandarua kwa kila atakakayepokea chandarua ili kuhakikisha kuwa tunafanikiwa kwa kiwango kikubwa.

"Niwaombe wanafunzi, wazazi na walezi kuzingatia elimu ya matumizi sahihi ya vyandarua ili kwa pamoja tufanikishe adhima ya kupunguza maambukizi kutoka asilimia nane hadi zero kwa mkoa na sisi kama ofisi ya mganga mkuu mkoa tutahakikisha tunapita  mitaani kufuatilia matumizi sahihi ya vyandadua hivi," alisema Nyalanja.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Wilaya ya Nyamagana Yonas Alfred akizungumuza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya hiyo ambapo ndiyo zoezi hilo limeanzia amewaomba wakazi wa wilaya ya Nyamagana na Mwanza kwa ujumla kuunga mkono na kuzingatia elimu ya matumizi sahihi ya vyandarua inayotolewa kwa wanafunzi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.