• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

VIJANA WATAKIWA KUTUMIA VETA KUPATA UJUZI KWA GHARAMA NAFUU NA KUJIAJIRI

Posted on: February 28th, 2025

VIJANA WATAKIWA KUTUMIA VETA KUPATA UJUZI KWA GHARAMA NAFUU NA KUJIAJIRI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ametoa wito kwa wazazi nchini kupeleka vijana wao kupata elimu na mafunzo ya ufundi stadi katika vyuo vya VETA nchini ili wapate ujuzi kwa gharama nafuu na kuweza kujiajiri.

Mhe. Mtanda ametoa wito huo leo  Februari 28, 2025 kwenye hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 30 ya utoaji huduma kwa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) yaliyofanyika katika viwanja vya chuo cha Mwanza.

"Leo tumeona katika maonesho ya vijana wetu jinsi gani wamepata ujuzi wa kutosha kwa fani mbalimbali jambo ambalo litawasaidia kujiajiri tena wamepata kwa gharama nafuu sana, natoa wito kwa vijana kutokaa vijiweni kuja kupata ujuzi." Mhe. Mtanda.

Akizungumzia darasa la madereva waliopewa ujuzi wa kuendesha magari na pikipiki amewataka vijana kufika kwenye vituo, kampasi na vyuo vya VETA nchini kwani kwa gharama nafuu ili kupata ujuzi utakao wasaidia kunusuru jamii kwa kuzuia ajali zinazoepukika.

"Zoezi la upandaji wa miti liwe endelevu kwenye taasisi na hata kwenye nyumba zetu kwani mabadiliko ya hali ya hewa yanategemea sana uhifadhi wa mazingira ili kutunza unyevunyevu na kusaidia hata kupatikana kwa maji kama kisima kilichokarabatiwa na VETA chenye umri mrefu." Amesema Mkuu wa Mkoa.

Awali, Mkurugenzi wa VETA Kanda ya ziwa CPA. Janeth Nyoni amesema kwa kipindi cha miaka 30 chuo kimekua na kuongeza vyuo hadi 11 tofauti na 3 vilivyokuwepo awali na kwamba kwa mwaka 2025 kanda hiyo imedahili jumla ya wanafunzi 5000 katika fani za muda mrefu na mfupi.

"Katika kuadhimisha miaka 30 ya utoaji huduma tumefanya shughuli mbalimbali kama kutoa mafunzo ya udereva bila malipo, kupanda miti, wanafunzi kuchangia damu, kukarabati majengo kwenye haspitali pamoja na kisima cha maji kwa wananchi wa kata ya Buswelu wilayani Ilemela." CPA Nyoni.

Mamlaka ya Elimu na Ufundi Stadi (VETA) ilianzishwa mwaka 1995 na sheria ya bunge namba 1 ya 1994 ambapo ina jumla ya vyuo 80 nchini na 11 vikiwa katika kanda ya Ziwa ambapo mwaka 2026 vitaongezeka 14 na kufanya jumla ya vyuo 25.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.