• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

VYAMA VYA USHIRIKA SIMAMENI IMARA KUONDOA UMASIKINI NCHINI: RC MAKALLA

Posted on: October 26th, 2023

VYAMA VYA USHIRIKA SIMAMENI IMARA KUONDOA UMASIKINI NCHINI: RC MAKALLA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla ametoa wito kwa vyama vya Ushirika nchini kusimama imara katika shughuli zao ili kuondoa umasikini na kuongeza ajira.

Akizungumza kwa niaba yake katika kilele cha siku ya Ushirika kwenye viwanja vya Furahisha ambapo kitaifa imefanyika Mkoani Mwanza, Katibu Tawala wa Mkoa huo Balandya Elikana amesema bado lipo kundi la Watanzania linaloishi katika hali ya umasikini hivyo kwa kupitia kazi za vyama vya Ushirika watakuwa mkombozi wa kuondokana na hali hiyo.

"Kwa mujibu wa Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 kuna kundi la Watanzania la asilimia 12 wanaoishi katika hali ya umasikini, ni matumaini yangu mipango imara ikifanyika kundi hilo litaondokana na umasikini kwa kupatiwa mikopo au shughuli za kujikwamua kiuchumi", Balandya.

Amevipongeza  vyama vya Ushirika kwa kupiga hatua wakianzia na mitaji midogo na kufikia mitaji mikubwa hadi Trilioni moja na kuwataka kuendelea kuheshimu kanuni na sheria zinazowaongoza.

"Ndugu mgeni rasmi  vyama hivi vya Ushirika vimekuwa vikifanya vizuri na mipango iliyopo sasa tumejipanga kuwa bora zaidi kwa upande wa Tehema ili shughuli zao zisambae hadi vijijini",Dkt.Abdulmajid Nsekeka,Mwenyekiti wa Tume ya kamisheni ya Ushirika Tanzania.

Akizungumzia hali ya vyama vya Ushirika nchini Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya vyama vya Ushirika Dkt.Benson Ndiege amebainisha hadi sasa wana mali yenye thamani ya Shs Trilioni 1.22 huku wakitoa mikopo ya Shs Trilioni 1.05

Katika kilele hicho cha ufungaji wa siku ya Ushirika,baadhi ya vyama vya Ushirika vilipatiwa tuzo mbalimbali kutokana na kufanya vizuri katka shughuli zao.

Kauli mbiu ya siku ya Ushirika mwaka huu inasema "Wanachama kusaidiana"

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.