• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Vyombo vya Habari vyakumbushwa kupeleka ujumbe sahihi kwa Wananchi

Posted on: August 18th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Adam Malima amewataka Waandishi wa Habari kutumia vyombo vyao kufikisha taarifa sahihi kwa wananchi hususani ujumbe wa masuala ya Afya ili kuwe na uelewa wa pamoja kwa mambo mbalimbali nchini.

Ametoa wito huo leo Agosti 18, 2022 wakati akifungua Semina ya mafunzo ya Uviko 19 kwa Waandishi wa Habari inayoratibiwa na Chama cha Waandishi wa Habari Mkoani humo kwa kushirikiana na Serikali kupitia Idara ya Afya ikilenga kuhamasisha chanjo ya ugonjwa huo kwenye jamii.

Mhe. Malima amebainisha kuwa kufikia Disemba 2022 Mkoa huo umelenga kuwafikia wananchi Milioni 2 wenye umri wa zaidi ya Miaka 18 kwa kuwapatia Chanjo ya Uviko 19 kupitia dozi rasmi zinazotolewa na Serikali hapa nchini.

"Ninayo taarifa ya mchango Mkubwa wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Mwanza kwenye Uhamasishaji wa Chanjo ya Uviko 19 kuanzia Uzinduzi na kampeni nzima ya kuhamasisha namna bora ya kuenenda ili kujikinga na maambukizi na hata kupambana na Matumizi ya dawa za kulevya, nawapongeza sana." Mkuu wa Mkoa.

Mwakilishi wa Muungano wa Klabu za Waandisbi wa Habari Tanzania (UTPC) Bi. Hilda Kileo amesema umoja huo unaendelea kuvilea vyama vya waandishi wa Habari Nchini na kwamba wanashirikiana na Serikali katika kuhakikisha jamii inapata Habari zilizo sahihi wakati wote.

Naye, Mwenyekiti wa Kilabu ya Waandishi wa Habari Mwanza, Edwin Nsoko amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa ushirikiano na amebainisha kuwa vyombo vya habari ni rafiki wa serikali na daraja la maendeleo nchini hivyo wataendelea kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kama mlezi wa chama hicho.

Aidha, Ndugu Nsoko amebainisha kuwa chama hicho ni mabalozi hodari kwenye kufikisha ujumbe wa Chanjo ya Uviko 19 kwa wananchi ili jamii itambue umuhimu wa chanjo hii kwa maslahi mapana ya afya zao na ustawi wa Taifa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.