• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WAFAYABIASHARA WA DAWA WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA ILI KUEPUKA KUMDHURU MWANANCHI: RC MTANDA

Posted on: May 17th, 2024

WAFAYABIASHARA WA DAWA WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA ILI KUEPUKA KUMDHURU MWANANCHI: RC MTANDA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka wafanyabiashara wa dawa kuepuka aina yoyote ya udanganyifu na badala yake wafuate Sheria na kanuni kutoka Mamlaka ya dawa na vifaa tiba TMDA.

Akizungumza leo Mei 17, 2024 eneo la Magereza, Butimba wakati wa hafla fupi ya kuwakabidhi msaada wa dawa kwa Jeshi hilo zilizotolewa na Mamlaka ya dawa na vifaa tiba (TMDA), Mtanda amesema bado wapo baadhi ya wafanyabiashara wanaofanya udanganyifu wa magendo na kuuza dawa zisizo sahihi hali ambayo inakuja kumdhuru mwananchi.

"TMDA nawapongeza kwa kuendelea kuonesha kuijali Jamii kwa kutoa msaada huu wa dawa zenye thamani ya shs milioni 56.4 kwa ajili ya Zahanati za Magereza,rai yangu kwenu kupitia wakaguzi wenu ongezeni bidii kuwabaini wale wote wanaofanya shughuli hii kinyume na utaratibu na wafikishwe kwenye vyombo vya kisheria,"Mkuu wa Mkoa

Aidha Mhe.Mtanda amezitaka Taasisi nyingine kuiga mfano wa TMDA wa kujali kuhudumia Jamii kwani kwa kufanya hivyo tunazidi kujenga jamii inayoishi kwa upendo na ushirikiano

Meneja wa Mamlaka ya dawa na vifaa tiba Kanda ya ziwa Mashariki,Sophia Mziray amebainisha huo ni utaratibu wao wa kila mwaka ambapo mwaka jana walitoa msaada wa dawa hizo wenye thamani ya shs milioni 58.

"Tunashukuru sana Taasisi hii kwa kuendelea kutujali,kama mjuavyo Jeshi letu lina shughulika na wafungwa na wanahitaji pia matibabu wanapokuwa wanatumikia vifungo vyao,msaada huu umelenga mahali mwafaka kabisa",Justin Kaziulaya,Mkuu wa Magereza,Mwanza.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.