• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WAHALIFU NA WANYANG’ANYI ZIWA VICTORIA KUTAFUTA SHUGHULI NYINGINE ZA KUFANYA

Posted on: September 16th, 2025

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imedhamiria kukomesha uharifu na unyang’anyi ndani ya ziwa victoria kwa nunua boti 11 za doria zenye thamani ya shilingi bilioni 4.5 huku Mkoa wa Mwanza ikipatiwa boti moja ambayo imegharimu shilingi milioni 400.

Akizungumza katika tukio la ushushwaji wa boti ya doria katika ziwa victoria Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesema Serikali inaendelea kuhakikisha inaimarisha usalama wa raia, mipaka, na mali za raia na Serikali itaendelea kufanya hivyo siku kwa siku.

Mkuu wa Mkoa amesema Mkoani Mwanza Serikali inajenga kituo kikubwa cha Utafutaji na Uokozi ndani ya Ziwa Victoria, ambapo kutakuwa na mtambo mkubwa wa mawasiliano utakaorahisisha mawasiliano ndani ya ziwa ikiwa ni mkakati unaotekelezwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki na muendelezo wa kuimarisha usalama ndani ya ziwa.

Mhe. Mtanda ameendelea kwa kusema serikali pia imenunua drone au ndege kubwa ambayo ina uwezo wa kuona sehemu kubwa ya ziwa na kubaini shughuli zote zinazoendelea ndani ya ziwa na vyombo hivyo vyote ni mali ya serikali na serikali ni moja.

“Lakini pia mnakumbuka tulileta ambulance boti kubwa kabisa, hivi vyote vitashirikiana kwa pamoja kufanya uokozi wa watu na mali zao ndani ya ziwa na mipaka yake”.

Naye, Mkuu wa Kikosi cha wanamaji Tanzania SACP Moshi N. Sokoro amesema boti hiyo ina vifaa vya kuongozea meli na mawasiliano na ni boti ambayo ina kasi sana, itahitaji utunzaji, awali amesema wamefanya mafunzo ya siku 2 kwa kuwa vifaa vilivyoletwa ni vya kisasa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza DCP Wilbroad Mutafungwa amesema kuendelea kupokea vifaa hivyo ni ishara kwamba uhalifu unakwenda kuisha kabisa kwa kuwa zitafanywa doria nyingi kwani vifaa wanavyo.

“Nitoe wito kwa wavuvi haramu na wanyang’anyi wanaofanya uhalifu ndani ya ziwa victoria waanze kutafuta shughuli nyingine za kufanya, wawaache wavuvi wafanye shuguli zao na wale wa vizimba wafanye kwa amani”. Amesema DCP Mutafungwa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA AWATAKA SHIMIWI KUTATUA MIGOGORO KUPITIA VIKAO

    September 16, 2025
  • WAHALIFU NA WANYANG’ANYI ZIWA VICTORIA KUTAFUTA SHUGHULI NYINGINE ZA KUFANYA

    September 16, 2025
  • RC MTANDA ASHUHUDIA USHUSHAJI WA VIVUKO MAJINI, WANANCHI VISIWANI MKAO WA KULA

    September 16, 2025
  • RC MTANDA AWAALIKA WALIOKOSA ELIMU RASMI KUJIUNGA NA MPANGO WA ELIMU WATU WAZIMA

    September 15, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.