• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WAKANDARASI WASIOKAMILISHA KAZI KWA WAKATI WASIPEWE ZABUNI-RAS MWANZA.

Posted on: September 17th, 2024

WAKANDARASI WASIOKAMILISHA KAZI KWA WAKATI WASIPEWE ZABUNI-RAS MWANZA

Katibu Tawala wa mkoa wa Mwanza Ndugu Balandya Elikana ametoa maagizo kwa Meneja wa Tarura wilayani Ukerewe kusimamia usiku na mchana ujenzi wa barabara ya RTC-Sungura ya km 0.62 inayotekelezwa na Mkandarasi Deep Construction Ltd kwa gharama ya zaidi ya shs milioni 400 kutokana na kuwa nyuma ya muda hadi sasa.

Balandya ameagiza pia wakandarasi wanaoonesha ubabaishaji wa kutekeleza miradi ya Serikali wasipewe zabuni au kusitisha mikataba waliyokubaliana kutokana na kurudisha nyuma kasi ya kuwaletea maendeleo wananchi.

"Sijalidhishwa hata kidogo na ujenzi wa barabara hii licha ya maelekezo niliyopatiwa,kazi ya miezi sita bado iko nyuma zaidi ya miezi tisa na fedha zimelipwa hii haikubaliki,"Katibu Tawala Mkoa.

Mtendaji huyo wa Mkoa amebainisha hayo leo Septemba 17,2024 wakati akiendelea na zoezi la ukaguzi wa miradi na kusisitiza Serikali inapenda kujenga uchumi wa nchi kwa kuwashirikisha watanzania wenyewe lakini baadhi ya wakandarasi wanakatisha tamaa kwa kupewa kazi ndogo na kushindwa kuikamilisha.

"Kazi hii imeshindwa kukamilika kwa wakati kutokana na changamoto ya hali ya mvua na jiografia ya wilaya hii maji yapo juu sana kutoka ardhini na tumeomba muda hadi mwishoni mwa Novemba mwaka huu,"Reuben Muyungi,Meneja Tarura,Ukerewe

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Mhe.Christopher Ngubiagai amebainisha maelekezo yote watayazingatia na wamejipanga kuhakikisha ujenzi huo unakamilika Novemba hii.


"Hizi ni fedha kutoka Serikali kuu na tayari zaidi ya shs milioni 165 zilizoombwa zipo mbioni kulipwa,sisi kama viongozi tuna wajibu wa kuzisimamia ipasavyo,"Mkuu wa Wilaya.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.