• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Wamachinga Mwanza wampongeza Rais Magufuli kupambana na Corona

Posted on: May 19th, 2020

Wamachinga mkoa wa Mwanza wafanya maandamano ya kumpongeza Mhe.Rais  Dkt.John Magufuli kwa mapambano dhidi ya ugonjwa wa homa kali ya mapafu COVID -19  tangu uingie nchini na kutowaweka watanzania kwenye zuio la kutotoka nje (lockdown).

Kauli hiyo ilitolewa kwa nyakati tofauti na na machinga hao akiwemo Mwenyekiti na Makamu mwenyekiti wa Shirika la Umoja wa Machinga Jiji la Mwanza, Said Tembo na Joseph Mwita wakati wakizungumza na waandishi wa habari wanasema wanaobeza  hatua ya Mhe. Rais kuwataka wananchi kuendelea kufanya kazi wapuuzwe.

Tembo alisema Machinga wanamuunga mkono Mhe. Rais Dkt. Magufuli kwa uamuzi wake mgumu na msimamo wa kutowaweka Watanzania kwenye zuio kwani alitambua umuhimu wa wananchi wake na kuwathamini .

Alisema kuwa Rais aliamini na kumtanguliza Mungu katika kupambana na corona kuliko binadamu wenyewe na kuna baadhi watu walitabiri Watanzania wengi watakufa kwa ugonjwa huo lakini hadi leo hata waliokuwa wameugua wamepona.

 “Wapo wanaombeza Mhe.Rais Dkt.Magufuli kuwa hakufanya jambo la busara kutowaweka Watanzania kizuizini hatupingi na tunatambua ugonjwa huo upo na hata yeye juzi akiwa Chato kanisani alisema katika kupambana na ugonjwa huo kila mtu anatumia mbinu yake.Hivi ukikaa ndani siku nne tu biashara hii ya kuingiza na kutoa mguu ndio ule hali ingekuwaje,”alihoji mwenyekiti huyo wa Machinga.

Alieleza kuwa laiti ingetokea ikawekwa karantini hakuna mfanyabiashara mdogo au mwananchi wa kipato cha kawaida mwenye bajeti ya kumudu kuendesha maisha kwa mwezi mmoja hivyo watanzania wana kila sababu ya kumpongeza na kumuunga mkono Mhe. Rais, amewawezesha kuendelea kuchapa kazi.

Kwa upande wake Makamu mwenyekiti wa Shirika hilo la Machinga, Joseph Mwita anasema wanamshukuru Mhe. Rais Dkt. Magufuli kwa alichokifanya kwa kuwatoa hofu wafanyabiashara na watanzania kuwa hakuna mtu wakufungiwa ndani huku akiwataka waendelee kufanya kazi kwa kujiamini ingawa corona ipo.

“Ametoa takwimu za mambukizi ya ugonjwa huo,ameyakabidhi  maisha ya wananchi na taifa kwa Mungu hivyo na sisi tumkabidhi kwa Mungu ampe maisha marefu huku tukichukua tahadhari na kufuata maelekezo ya serikali na wataalamu wa afya,”alisema Marwa.

Aidha, mjasiriamali katika Soko Kuu la Mwanza, Ester Mgaya alisema hawana budi kumshukuru Mungu lakini pia Rais kwa uamuzi wake mgumu wa kuwatoa hofu watanzania wasitishwe na corona yakuwa hali ikiendelea hivi ataruhusu vyuo vifunguliwe na kushauri kuendelea kumwomba Mungu ili corona itokomee.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.