• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Wamiliki wa Biashara za Vileo watakiwa kuzingatia Sheria na Kanuni za Uendeshaji Biashara

Posted on: May 22nd, 2023

*Wamiliki wa Biashara za Vileo watakiwa kuzingatia Sheria na Kanuni za Uendeshaji Biashara**


Katika kuhakikisha kwamba biashara za Vileo zinafanyika kwa amani na utulivu, Wamiliki wa Biashara hizo wametakiwa kuzingatia Sheria na Kanuni za uendeshaji wa biashara hizo kwani kwa kukiuka kufanya hivyo na kuzalisha  kelele sumbufu, watachukuliwa hatua kwa mujibu wa taratibu za Baraza  la Taifa la Usimamizi wa Mazingira NEMC.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya llemela Mhe.Hassan Masalla, akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza leo Mai 22, 2023  katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, alipokutana na Vyombo vya Habari.

 Mhe.Hassan Masalla amebainisha kuwa Mkoa wa Mwanza kwa kushirikiana na NEMC Mei 5, 2023 walifanya zoezi maalum la kaguzi 50 za wafanyabishara za Vileo na kubaini maeneo 31 ya biashara za vileo  kwenda kinyume na Sheria na kuchukuliwa hatua na kupewa maelekezo namna ya kudhibiti kelele hizo sumbufu.

"Ndugu zangu waandishi nawaomba muwaelimishe vyema wananchi kuhusiana na Sheria na Kanuni za kudhibiti kelele sumbufu, baadhi yetu tumekuwa siyo rafiki na hali hii kutokana na sababu mbalimbali, Serikali inaheshimu taratibu zote zilizowekwa, Biashara hizi zilizobainika kukiuka Sheria zimepigwa faini kati ya Milioni 2 hadi 5 huku zikiendelea kutoa huduma nyingine kama kawaida," amefafanua Mhe.Masalla.

Aidha, amebainisha kuwa maeneo ya biashara za vileo zilizotozwa faini ya Shilingi Milioni 5 ni zile zilizobainika kuwa sugu kwa kuzalisha kelele sumbufu licha ya kuonywa mara kadhaa,na sasa zimetakiwa kuweka vifaa maalum vya kudhibiti kelele hizo.

"Tumejitahidi kuwapa ellimu ya kutosha licha ya kuwapa adhabu kwa mujibu wa kanuni zetu,tunashukuru sasa wamepata uelewa mzuri ili mwisho wa siku kusiwepo na kero kati ya anaye starehe na aliyepo nje na eneo la starehe,"Jerome Kayombo,Meneja Mkoa NEMC.

Aidha Mhe.Masalla amesema zoezi la ukaguzi wa nyumba za ibada litafuata baada ya kukamilika taratibu maalum kwani siyo rahisi kufanya kwa pamoja kaguzi za sehemu za vileo na nyumba za ibada.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.