• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Wananchi wa Chasarawi Wilayani Kwimba watumia nguvu zao kujiletea maendeleo

Posted on: March 3rd, 2023


Wananchi wa Kijiji cha Chasarawi katika Kata ya Bupamwa wilayani Kwimba wamechangishana na kununua eneo la ardhi lenye ukubwa wa Hekari nane kwa ajili ya kujenga Shule ya Msingi ili kuwapunguzia watoto adha ya kutembea umbali mrefu wa zaidi ya Kilomita tano.


Hayo yamebainishwa leo wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe Adam Malima ambapo kiongozi huyo amekagua na kuweka Jiwe la Msingi kwenye ujenzi wa Miundombinu ya vyumba vya Madarasa 9,  Matundu ya Vyoo 30 na Jengo la Utawala kwenyw shule ya Msingi Mwalulyeho yanayotekelezwa kwa Tshs. Milioni 150 zilizotolewa na serikali kuu.

Amesema, wananchi wa kijiji hicho wameonesha kuwa na kiu ya maendeleo na uzalendo kwa kuamua kwa hiyari kununua eneo na kuanzisha ujenzi kabla ya serikali kuwaletea mawazo na akatumia wasaa huo kuwaahidi kuwatimizia ndoto yao ya kupata shule kwa kuhakikishia kukamilika kwa ujenzi mapema mwezi Aprili 2023.

"Nawashukuru sana kwa kujitolea kuanzisha mradi wa maendeleo na ukiona jamii inafanya haya kwa hiyari basi ujue eneo hilo wananchi wake wanajitambua sana maana hakuna mtu anayeweza kujenga shule ili asome mwanae pekee bali ni kwa ajili ya jamii nzima., hongereni sana." Malima.

Aidha, ametoa rai kwa wazazi wa kata ya Bupamwa kuhakikisha wanawapeleka watoto shule hususani wa kike ili kuwatimizia ndoto ya kujitegemea na akawasihi kuacha tabia ya kuwaozesha kwa kishawishi cha kupata mifugo kama mahari huku akisema wakifanya hivyo wataharibu jamii nzima ya sasa na baadae.

Naye,  Mkuu wa Wilaya ya Kwimba Mhe. Ngw'ilabuzu Ludigija ametumia wasaa huo kumshukuru Mhe Rais kwa kuwaletea fedha za ujenzi wa shule hiyo na akawapa kongole wananchi kwa kuamua kujiletea maendeleo wenyewe bila kusubiri na akawataka kuendelea na tabia hiyo njema.

"Rais Samia hakukosea kukuleta Mhe. Malima Mkoani Mwanza maana tutanufaika sana na Uongozi wako maana una uchungu wa maendeleo ndio maana pamoja na kufanya ziara za kusikiliza kero za wananchi unahakikisha unakagua kila mradi hadi iliyopo maeneo ya mbali kiasi hiki." Me. Sabana Salinje, Mwenyekiti wa CCM Magu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kwimba Mhe. Thereza Luhangija amewapongeza wananchi kwa kujitolea kuanzisha mradi huo kwa kiu ya maendeleo yao wenyewe na akatoa wito kwao kutunza miundombinu hiyo ili iwasaidie vizazi vya sasa na baadae.

Awali, Mhe. Mkuu wa Mkoa amefika kwenye kata ya Mwamitinje na kukagua Ujenzi wa vyumba 3 vya madarasa na matundu 6 ya vyoo kwa zaidi ya Tshs. Milioni 84 chini ya mradi wa kupunguza umasikini (TASAF) na akawasihi kamati ya Ujenzi kufanya kazi hiyo kizalendo na yeyote atakayehujumu ujenzi huo atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Hata hivyo, Mkuu wa Mkoa akiwa eneo la hifadhi ya Maji ya Bonde Kwimba, ameagiza ufanyike utambuzi na uhakiki wa mipaka ili kupata suluhu ya mgogoro kati ya wananchi na Mamlaka ya bonde la ziwa Victoria.

Amesema timu ya Mkoa, Bonde la Maji ya ziwa Victoria na Halmashauri watakuja na ramani ya mwaka 1958 ili kujiridhisha kama wananchi wanaodai kuporwa ardhi yao wako ndani ya hifadhi ama laa na amewataka waje na wataalam wa ramani ili wasije kudai kuwa walilazimishwa.

Katika nyakati tofauti Mhe Mkuu wa Mkoa ameziagiza RUWASA, TANESCO, REA kupeleka huduma kwenye miradi ya VETA inayotarajia kuanza Julai mwaka huu, Kituo cha Afya Hungumarwa ambacho amekizindua rasmi kwa ajili ya kuanza kutoa huduma mwezi Aprili.

Kabla ya kuhitimisha ziara kwa kuzindua mradi wa Maji wenye thamani ya Milioni 650 kwenye kijiji cha Ngula na kuwataka wananchi kuutunza,ziara ya Mhe. Malima imemfikisha kwenye Shamba la Hekari 2.5 la bwana Gogomoka Mkonongo lililopo kwenye kijiji cha Ligembe ambaye amepanda kitaalamu kwa kufuata sheria bora za kilimo huku akiwa akitumia mbolea ya samadi na akawaagiza maafisa Ugani kutoa Elimu ya Kilimo bora.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.