• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WANANCHI WA HUNGUMALWA KWIMBA WAPATA MRADI MKUBWA WA MAJI WA ZAIDI YA BILIONI 10

Posted on: November 28th, 2023

WANANCHI WA HUNGUMALWA KWIMBA WAPATA MRADI MKUBWA WA MAJI WA ZAIDI YA BILIONI 10


*RC Makalla amshukuru Rais Samia kwa kutenga fedha zaidi ya Bilioni 10 kutekeleza mradi huo*


*Awataka wananchi kulinda miundombinu ya maji na kuumiliki mradi huo kupitia jumuiya ya watumia maji*


*Amemtaka Mkandarasi kukamilisha ujenzi wa mradi huo kwa mujibu wa mkataba*


*Awataka Kamati ya Siasa na Mkuu wa Wilaya hiyo kuendelea kufuatilia mradi huo*


*Abainisha kuwa wananchi zaidi ya elfu 24 watanufaika na mradi*


*Amewasihi wananchi kuacha kutumia maji ya Ziwa badala yake watumie maji safi na salama ya bomba*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. CPA Amos Makalla leo Novemba 28, 2023 amekagua mradi mkubwa wa maji unaojengwa na Emirates Builders Company Ltd kwa zaidi ya Bilioni 10.8 kwenye Kata ya Hungumalwa wilayani Kwimba.

Akizungumza na wananchi baada ya ukaguzi huo CPA Makalla ametumia wasaa huo kumshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutenga fedha zaidi ya Bilioni 10.8 kujenga mradi huo ambao hadi sasa umetekelezwa kwa asilimia 80 huku ukikusudiwa kunufaisha zaidi ya wananchi elfu 24.

Makalla amesema akiendelea na ziara yake wilaya ya Kwimba ambayo ameianza Novemba 27, 2023 amebaini pamoja na miradi mingine kuna miradi mikubwa mitatu ya maji tena kwenye vijiji vya mbali jambo ambalo ni ishara ya adhma ya nia njema ya Serikali kuwapatia wananchi maji safi na salama.


Aidha, amewasihi wananchi kuacha tabia ya kutumia maji ya ziwa na badala yake amewataka kutumia maji safi ya bomba pamoja na kuhakikisha wanalinda miundombonu ya miradi hiyo pamoja na kuimiliki kupitia jumuiya ya watumia maji ili iweze kuwasaidia kwa muda mrefu.


Akizungumza kwa niaba ya wananchi, Mkuu wa Wilaya ya Kwimba Ng'wilabuzu Ludigija amemshukuru Rais Samia kwa kuwaletea mradi huo wananchi ambao awali wamekua wakitumia maji ya ziwa yaliyowapelekea kuugua magonjwa ya tumbo na ametoa rai kuunganisha maji kwenye nyumba zao kwani ni watu 490 tu wameunganishwa.

"Mradi huu unaotumia chanzo cha bomba kuu la KASHWASA utasaidia kuwapatia wananchi wa Hungumalwa maji safi kwa asilimia 100 hususani katika kata ya Ilula ambao kwa sasa wanapata maji kwa asilimia 50 tu" Amefafanua Meneja wa RUWASA (W) Mhandisi Godliver Gwambasa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.