• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Wataalam wa Maabara Mwanza wakumbushwa kutoa huduma bora na kuzingatia miiko ya kazi

Posted on: April 25th, 2023


Wanachama na wadau wa Chama cha  Wanasayansi wa Maabara za Afya Tanzania (MeLSAT) Mkoa wa Mwanza  wametakiwa kushiriki kikamilifu shughuli mbali mbali za chama kama njia ya kuendelea kudumisha huduma kwa  wananchi

Wito huo umetolewa  leo Aprili 25 2023 na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana wakati akifungua Maadhimisho ya Wiki ya  Wataalam wa Maabara Mkoa wa Mwanza katika viwanja vya Furahisha Wilaya ya Ilemela.

Bw. Balandya ameongeza kuwa wadau na  wataalam wa maabara watumie maadhimisho hayo kama njia ya kuboresha huduma  katika Mkoa wa Mwanza na Tanzania kwa ujumla.

"Nitoe wito kwa wataalam wote wa Maabara Mkoa wa Mwanza kuwa wanachama hai wa Chama cha Wanasayansi wa Maabara za Afya Tanzania (MeSALT) na kushiriki katika shughuli mbali mbali za chama pia Waajiri  mtoe ruhusa kwa Wataalam wa Maabara kushiriki shughuli za chama bila kuathiri utoaji huduma kwa wananchi," Amesema Mtendaji huyo wa Mkoa

Aidha  Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt. Thomas Rutachunzibwa amesema Mkoa wa Mwanza unaendelea kuhakikisha kuwa huduma za afya zinazotolewa zinakuwa bora kwa kusimamia ubora wa huduma za maabara za Serikali na za watu binafsi.

"Mkoa wa Mwanza kupitia timu ya usimamizi wa huduma za afya  tunaendelea  kusimamia na kuhakikisha kuwa huduma zote za afya zinazotolewa zinakuwa bora kwa kusimamia ubora wa huduma za maabara za Serikali na watu binafsi," amesema Rutachunzibwa

Pia Mwenyekiti wa Chama cha Wanasayansi wa Maabara za Afya Tanzania (MeSALT)  Bertrand Msemwa amesema anaiomba serikali kuendelea kuajiri wataalam wa Maabara ili waweze kufanya kazi katika kiwango ambacho kinatakiwa na huduma ziweze kutolewa nzuri.

Naye Katibu wa Chama cha Wanasayansi wa Maabara za Afya Tanzania (MeLSAT) Mkoa wa Mwanza Bw. Yusuphu Mkama amesema  wananchi wa Mkoa wa Mwanza  wafike sehemu maadhimisho yanapofanyika ili waweze kupatiwa huduma  za vipimo bure.

"Niwaombe wananchi wa Mkoa wa Mwanza muweze kufika mahali hapa ambapo maadhimisho yanafanyika muweze kupatiwa huduma na kujua afya zenu kwakuwa huduma za vipimo ni bure,"amesisitiza Mkama

Maadhimisho hayo yamefanyika Ki- Mkoa kwa mara ya 2 ikiwa ni maadhimisho ya 12 tangu kuanzishwa ambayo yanafanyika kwa muda wa wiki moja kuanzia Aprili 24  hadi Aprili 28 2023.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.