• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WAZIRI DKT. NDUMBARO AWATAKA WALIONG'ARA UMISSETA NA UMITASHUMTA WAITWE TIMU YA TAIFA MASHINDANO YA FEASSSA

Posted on: July 1st, 2024

WAZIRI DKT. NDUMBARO AWATAKA WALIONG'ARA UMISSETA NA UMITASHUMTA  WAITWE TIMU YA TAIFA MASHINDANO YA FEASSSA


Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amemtaka Mkurugenzi Msaidizi wa michezo Dkt. Ado Komba kuhakikisha anawaingiza wachezaji hodari na wenye vipaji kutoka Mkoa wa Mwanza waliofanya vizuri katika mashindano ya UMITASHUMTA na UMISSETA 2024 yaliyofanyika Mkaoni Tabora kuingizwa kushiriki katika mashindano ya shule za nchi za Afrika Mashariki (FEASSSA) yatakayofanyika nchini Uganda.

Wanamichezo hao ni Neema Mkula ambaye alikuwa mfungaji bora mpira wa pete mashindano ya UMITASHUMTA akiwa na jumla ya magoli 360,  Magreth Manawa mfungaji bora mpira wa kikapu UMISSETA ana jumla ya vikapu 110 pamoja na Agnes John mfungaji bora mpira wa pete ana jumla ya magoli 290.

Mhe. Dkt. Ndumbaro ametoa agizo hilo leo Julai 01 2024, alipokuwa akizungumza wakati wa kukabidhi jumla ya makombe 31 kwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda  (12 kwa UMITASHUMTA na 09 kwa UMISSETA), Aidha Mkoa wa Mwanza ulifanikiwa kuwa mshindi wa jumla kwanza katika mashindano ya UMITASHUMTA na UMISSETA Kitaifa 2024.

Waziri huyo wa Michezo amesema wanafunzi hao wamefanya vizuri na kwa kuwa michezo hiyo imechezwa hadharani na ulikuwa mchezo wa wazi hivyo wamekidhi kuchaguliwa kushiriki kwenye mashindano ya Shule za Nchi za Afrika Mashariki (FEASSSA) yatakayofanyika nchini Uganda.

Waziri Ndumbaro amesema michezo ni ajira na  michezo ni uchumi, hivyo ukiona una kipaji au una umahiri wa mchezo wowote ule basi hakikisha unanakiendeleza kipaji hicho kwani zama zimebadilika sana, unaweza kuajiriwa kupitia kipaji hicho.

"Hapa nchini kuna wachezaji wanalipwa mil. 50 kwa mwezi hata mimi Waziri Ndumbaro na RC hapa hatufikii hata robo hivyo ukiona una kipaji kiendeleze maana ni ajira".Waziri Ndumbaro

Amesema UMITASHUMTA na UMISSETA ndio chimbuko la mafaniko kwa vijana wengi watakaokuja kuwa wachezaji wakubwa na ambao pia watakwenda kushiriki katika michuano mbalimbali kimataifa,hivyo hatuna budi kuviachilia vipaji vyetu vikapotea wakati huo tayari ni mtaji.

Aidha Dkt. Ndumbaro amesema Tanzania inatarajia kuandaa mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027, hivyo amewataka wale wote wanaofanya skauti ya wanamichezo kuhakikisha wanawaibua wachezaji mahiri na hodari ili waweze kushiriki katika Timu ya Taifa.

"Hatuwez kuvuna bila kupanda, lazima tupande ndipo tuvune na sasa ndio wakati mzuri wa kuwaandaa vijana wetu ili ifikapp 2027 tuwe na timu nzuri ya mashindano",Waziri Ndumbaro

Naye Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewawapongeza wanamichezo wote kutoka Mwanza kwa heshima kubwa waliouletea Mkoa huo, kwani wameuheshimisha kwa kuleta makombe mengi.

Aidha Mhe. Mtanda ametoa maagizo kwa Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana kupitia kwa Afisa Elimu na Utamaduni kwa wale wanafunzi wote 18 waliofanya vizuri kuhakikisha wanapata zawadi ili iwawahamasishe hata wengine.

Agizo hilo tayari limetekelezwa na wale wote waliofanya vizuri katika mashindano hayo wamepatiwa zawadi ya fedha taslimu kiasi cha Tsh. Laki moja kwa washindi, wachezaji bora, hodari na waliochaguliwa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.