• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Waziri Jaffo asisitiza ukusanyaji wa mapato

Posted on: October 22nd, 2018

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)Mhe. Suleiman Jaffo amewataka watendaji kuongeza  kasi ya ukusanyaji wa mapato wa Manispaa ya Ilemela, ambayo ni miongoni mwa manispaa zenye vyanzo vingi vya mapato.

Jaffo ameyasema hayo wakati alipokuwa akizungumza na watendaji na wafanyakazi wa Manispaa ya Ilemela ambapo alipata fursa ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya afya na barabara ambayo inatekelezwa chini ya Wizara yake,  wakati wa ziara yake ya kikazi ya siku moja katika manispaa hiyo.


Kwenye mkutano wake na watumishi wa manispaa hiyo, Jaffo aliwasimamisha Mchumi wa Manispaa hiyo Amosy Zephania na Mtunza Hazina wa Manispaa hiyo Jamea Dalasia ili  kueleza mikakati waliyoweka kuhakikisha nakusanya mapato na kufikia malengo waliyoweka kama Manispaa.

“ Kwenye suala la ukusanyaji wa mapato, nilichokigundua kwa baadhi ya maeneo mengi ni uzembe wa baadhi ya watumishi na msikubali mtu mmoja akawaharibia kazi”, alisema Mhe.Jaffo.

Alimtaka Mkurugenzi Mtendaji wa manispaa ya Ilemela John Wanga kuwa mkali na kuhakikisha kuwa anawachukulia hatua kali baadhi ya watumishi walio chini yake wenye malengo ya kukwamisha juhudi za ukusanyaji wa mapato.

“ Kamati ya fedha na mipango simamieni vizuri  ukusanyaji wa mapato ya manispaa yenu, makosa ya mtu mmoja yanaweza kusababisha manispaa yenu kusemwa vibaya,"alisema Mhe.Jaffo.

“ Unapoona manispaa yenu inasemwa vibaya, maana yake unaharibu jina la Mkuu wa Mkoa, Mkuu wenu wa wilaya na kamati nzima ya fedha,tubadilike na tuache kufanya kazi kwa mazoea."


Katika hatua nyingine Jaffo alimpongeza Mkurugenzi Mtendaji wa manispaa hiyo John Wanga kwa kufanya maboresho ya ukusanyaji wa mapato kwenye Soko la Kimataifa la Mwaloni ambapo makusanyo yamepanda kutoka Sh milioni 34 hadi kufikia Sh. milioni 54  katika kipindi cha kuanzia Oktoba mosi hadi Oktoba 21 mwaka huu.

 Kwa mujibu wa Wanga, ufanisi huo wa ukusanyaji wa mapato katika soko hilo, umetokana na manispaa hiyo kununua mizani ya kisasa ya kupimia mazao ya samaki, hali ambayo imeongeza mapato hayo maradufu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.