• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WAZIRI KIKWETE ATOA ZAWADI KWA SHULE/WALIMU WALIOFANYA VIZURI KITAALUMA MWANZA

Posted on: September 26th, 2024

WAZIRI KIKWETE ATOA ZAWADI KWA SHULE/WALIMU WALIOFANYA VIZURI KITAALUMA MWANZA


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Ridhiwani Kikwete ameipongeza Serikali ya Mkoa wa Mwanza kwa kujiwekea mkakati mzuri wa kuzipongeza halmashauri, walimu na shule za msingi na sekondari zilizofanya vizuri katika mitihani ya kujipima ya Mkoa.

Ametoa pongezi hizo wakati akizungumza na wakuu wa shule pamoja na wadau wa elimu  katika kikao kilichofanyika kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza leo Septemba 26, 2024,na kuongeza kuwa motisha hiyo iwe chachu ya kufanya vizuri zaidi.

Aidha Mhe. Kikwete amezipongeza Halmashauri za Kwimba na Sengerema kwa kufanya vizuri na kuongoza Halmashauri zingine kwenye mitihani ya kujipima ya Mkoa kwa shule za msingi na sekondari,kitendo ambacho kinaonesha kumuunga mkono kwa vitendo Mhe.Ris Dkt.Samia Suluhu Hassan ambaye ametoa fedha nyingi katika sekta ya elimu nchini

"Kwa upekee kabisa niipongeze sana wilaya ya kwimba na Sengerema kwa kuvunja rekodi ukiachilia wilaya za Ilemela na Nyamagana ambazo ndio zilikua zikishindana lakini mwaka huu wamepata ushindani". Amesema Mhe. Kikwete wakati akizungumza na na viongozi hao

Naye Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amemuagiza Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza na Afisa elimu kukaa na kupanga mikakati ya motisha za juu lengo likiwa  Mkoa huo uzidi kung'ara katika ufaulu wa wanafunzi kuanzia kimkoa hadi Taifa.

"Maafisa elimu chini ya Katibu Tawala wakakae waboreshe nyaraka hii inayoonesha mkakati wa Mkoa katika kuboresha elimu halafu tuweke siku maalumu na wadau wa elimu ya kuuzindua kuelekea mwaka 2025". Amesema Mhe. Mtanda.

Kikao hicho cha utoaji wa zawadi kwa Halmashauri, Walimu na shule za sekondari na msingi kimeambatana na zoezi la kukabidhi madawati  Arobaini (40) kwa shule ya Msingi Uhuru iliyopo Wilaya ya Nyamagana kata ya Igoma iliyokabiliwa na upungufu huo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.