• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Waziri Mchengerwa aagiza miradi ya afya Sengerema ianze kutoa huduma haraka

Posted on: December 16th, 2023

Waziri Mchengerwa aagiza miradi ya afya Sengerema ianze kutoa huduma haraka


Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Tamisemi, Mhe. Mohamed Mchengerwa ameagiza  vituo vya afya vilivyopo wilayani Sengerema vianze kutoa huduma haraka kwa wananchi.

Akizungumza leo kwenye kituo cha afya kilichopo kijiji cha Kanyerere kilicho chini ya mradi wa Tasaf kilichofika asilimia 96 lakini hakijaanza kutoa huduma, Waziri Mchengerwa amesema haoni sababu ya msingi ya kuwacheleweshea huduma wananchi licha ya kupewa maelezo ambayo hayakumridhisha.

Amebainisha maelezo yote aliyopatiwa kuhusu kituo hicho yameonesha waliopewa dhamana ya kusimamia wameshindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo hivyo ametoa wiki mbili kituo hicho na vingine 11 viwe vimeanza kutoa huduma.

"Katibu Tawala wa Mkoa nakuagiza simamia ipasavyo zoezi hili waandikie barua wahusika wote ili mradi huu uanze kazi,hatuna sababu ya kuwapa hasira wananchi wetu kituo wanakiona lakini wanaendelea kuteseka kupata hudum seea za afya,"Mhe Mchengerwa.

"Mhe Waziri kwa mujibu wa taratibu za Tasaf mradi huu wananchi walitakiwa kuchangia asilimia 10 na Tasaf asilimia 90,sasa kuna baadhi ya vijiji vimesua sua kuweka nguvu zao ndiyo maana mradi huu umechelewa kuanza kwa wakati,"Binuru Shekidele,Mkurugenzi Halmashauri ya Sengerema.

"Kituo hiki kimegharimu shs milioni 481 kuna upungufu wa shs milioni 35 ili kiweze kutoa huduma kwa wananchi,bado hatujaingiza umeme na maji,"Malisa Ndugha,mratibu wa Tasaf ,Sengerema

Mbunge wa Jimbo la Sengerema Mhe.Hamis Tabasamu amesema bado baadhi ya vijiji wanafunzi wanalazimika kutembea umbali wa km 18 kwenda shule, amehakikishiwa na Waziri Mchengerwa shule zote zilizoanzishwa kwa nguvu ya wananchi jimboni kwake na zimeishia hatua ya boma Serikali itazigharamia kuzikamilisha.

Waziri Mhe Mohamed Mchengerwa aliyesimama kwa muda mfupi wilayani Sengerema akitokea Mkoani Geita kuja Mwanza, amesema Serikali imeunda timu ya wakaguzi wa miradi ya elimu na afya watakaozunguka nchi nzima kufanya tathmini ya miradi hiyo na kutoa ushauri kwa Setikali.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.