• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa mgeni rasmi Wiki ya nenda kwa Usalama Barabarani Kitaifa Mwanza

Posted on: March 13th, 2023


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (MB) anatarajiwa kuwasili Mkoani Mwanza Jumanne Machi 14, 2023 kwa ajili ya Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama barabarani Kitaifa yatakayofanyika kwenye Viwanja vya Furahisha.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Kighoma Malima wakati wa Mkutano na Waandishi wa Habari uliofanyika kwenye Ukumbi wa Ofisi ya Mkoa  mapema leo Jumatatu Machi 13, 2023 ambapo amesema Mhe. Waziri Mkuu atakua Mgeni Rasmi kwenye Ufunguzi wa Juma hilo ambalo litaadhimishwa katika Mikoa yote nchini.

Mhe. Malima ametumia wasaa huo kuwakaribisha wananchi wa Mwanza na Mikoa ya jirani kujitokeza kwa wingi  kandokando ya barabara ya Uwanja wa ndege na kwenye viwanja vya Furahisha vilivyopo wilaya ya Ilemela ili pamoja na kumlaki na kumpokea Kiongozi huyo wapate  Elimu ya Sheria, Kanuni na Taratibu za Usalama barabarani.

Ameongeza kuwa, katika Mkoa wa Mwanza takwimu za ajali kwa kipindi cha mwaka mmoja uliopita (Januari-Disemba 2022) zimeripoti jumla ya ajali kubwa 81, zilizosababisha vifo vya watu 71 na kujeruhi watu 96. Aidha, kwa upande wa Pikipiki zimetokea ajali kubwa 30 zilizosababisha vifo vya watu 25 na kujeruhi 26.

"Mwelekeo wa takwimu hizo sio mzuri kabisa, niwatake watumiaji wote wa Barabara katika Mkoa wa Mwanza kuzingatia Sheria na kanuni za Usalama barabarani. Vitendo vinavyoongoza sana katika kusababisha ajali hizi pamoja na Mwendokasi, ubovu wa vyombo vya Moto, Ulevi, Kulipita gari mbele bila kuchukua tahadhari, ujazaji wa abiria na mizigo uliopitiliza na kuegesha magari yaliyoharibika barabarani." Mhe. Malima.

Vilevile ameongeza kuwa Mkoa wa Mwanza una kaulimbiu ya kudumu kuhusu Usalama barabarani isemayo (Karibu Mkoa wa Mwanza, tafadhali zingatia sheria na kanuni za usalama barabaran, Epuka adhabu kali)

na akatoa wito kwa watumiaji wa vyombo vya moto kuchukua tahadhari ili kuepusha ajali.

Mhe. Malima amebainisha kuwa Maadhimisho hayo ya Kitaifa mwaka huu yanakwenda sambamba na Kauli mbiu isemayo 'Tanzania bila Ajali inawezekana, Timiza wajibu wako' na kwamba kauli mbiu hiyo inasisitiza kuwa kila mtumiaji wa Barabara akitimiza wajibu wake kutapelekea kupungua kwa ajali za Barabarani na hatimaye kuimarika kwa Usalama barabarani.

Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Usalama barabarani Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ramadhani Ng'anzi ametoa wito kwa wamiliki wa vyombo vya moto kufika katika vituo vya polisi vilivyotengwa kwa ajili ya ukaguzi wa vyombo vyao na baada ya ukaguzi watapata cheti maalumu cha kufuzu kutumia barabara na kwamba Serikali imejipanga kuona kwamba katika matumizi ya barabara kitu cha kwanza kinachozingatiwa ni usalama.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.