• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Waziri Mkuu Majaliwa aridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa Meli MV Mwanza

Posted on: October 18th, 2022


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa  Oktoba 17, 2022 amefanya ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa meli ya Mv Mwanza Hapa Kazi Tu inayojengwa katika bandari ya Mwanza Kusini Wilaya ya Nyamagana Mkoani Mwanza na kuridhishwa na hatua ya ujenzi huo ambao umefikia asilimia 73.

 Akizungumza na wananachi pamoja na viongozi wa mkoa wa Mwanza baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa meli hiyo  Mhe. Majaliwa amesema amefurahishwa na mwenendo wa kazi unaoendelea na kwamba  kampuni ambayo serikali ilingia nayo mkataba wa ujenzi wa meli hiyo ya  GAS Entec ya Korea Kusini ipo, wafanyakazi wote wapo na  watanzania waliokuwa wamepunguzwa wapo.

Ikumbukwe kamba Mei 7, 2022 Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa akiwa Mkoani Mwanza kwa ziara ya siku moja ya kikazi alikagua ujenzi wa meli hiyo na kutoridhishwa kabisa na maendeleo yake ambayo ilikuwa imefikia asilimia 65 huku mkandarasini wa kampuni ya GAS Entec ya Korea Kusini akiwa  ameuza hisa zake bila kuitaarifu serikali.

 Pia serikali ilikuwa imeishamlipa  mkandarasi asilimia 80 ya gharama za ujenzi wa meli hiyo lakini kampuni aliyoiuzia hisa zake ilikataa kutambua ujenzi wa meli kwa madai kwamba swala hilo liko nje ya mauziano, vilevile alikuwa amepunguza wafanyakazi kutoka 118 hadi 22.

 Dosari hizo zilimfanya Mhe, Majaliwa kumuagiza Afisa Uhamiaji wa Mkoa wa Mwannza akamate pasi za kusafiria za wataalamu wa Kampuni hiyo ya GAS Entec hadi wakamilishe kazi yao.


Amesema asilimia 73 zilizofikiwa ni mwenendo mzuri na mhandisi  mtanzania anayesimamia mradi huo amemhakikishia kwamba dosari zote zilizokuwepo awali hazipo sasa, wanachapa kazi na kwamba mafanikio hayo yametokana na  maamuzi ambayo serikali ilichukua ya kuwanyang’anya pasi za kusafiria.

“Najua kuna Watanzania walikasirika ooo wawekezaji mmewanyang’anya hati zao za kusafiria  mlitaka watoroke watuachie mradi mkubwa hivi halafu ningekuwa mgeni wa nani ilitulazimu kakaa chini na nchi yao kupitia Balozi wao tukaelezana tukakubaliana kwanza kampuni iliyouza hisa zake ambayo tuliingia nayo mkataba isiondoke, yenyewe ndiyo ijenga hadi ikamilishe ujenzi wa meli yetu na wafanyakazi wote kutoka kwao walioondoka warudishwe nchini, waje waendelee na kazi yao pia wafanyakazi wa Tanzania 112 waliofukuzwa kazi warudishwe kazini na kazi ikamilike,”ameeleza

 Mhe. Majaliwa amesema baada ya makubaliano mkandarasi huyo aliahidi kumaliza kazi ya ujenzi wa meli  Mwezi wa 11 na itabaki kazi ndogo hivyo ameagiza muda huo ukifika  iingizwe ndani ya maji kwa ajili ya kukamilisha shughuli ambazo zinatakiwa zikamilishwe meli ikiwa majini.

“Kwa ujumla leo hii nimeridhishwa na kazi inayoendelea hapa kwenye ujenzi huu wa meli hii nimeenda hadi huko uvunguni, kwenye chumba cha kukaa captain  mashine zipo na wanaendelea na kazi, watanzania muamini kwamba kazi hapa inaenda vizuri msisitizo ni ule ule kwamba lazima kazi ikamilike kwa asilimia 100 na uzuri hadi hapo walipofikia hawatudai bali sisi ndiyo tunawadai meli," ameeleza.

“Kama alivyoagiza  Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwamba kazi iendelee nawahakikishia wananchi na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi mliopo hapa  miradi yote itakamilika kwa wakati na mingine itaongezwa tuko kazini muda wote hakuna mradi utakaokwama.


“Nirudie kutoa wito kwa wasaidizi wote wanaomsaidia kazi Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan mawaziri, makatibu wakuu, wakuu wa mikoa , wakurugenzi, wakuu wa wilaya na wengine wote tuchape kazi ili watanzania waone faida ya uwepo wa serikali yao, nirudie tena kuwahakikishia wana CCM hakuna mradi ambao utashindwa kutekelezwa kwa sababu wasaidizi wa Mhe.Rais tumejipanga kuisimamia vizuri,”amesisitiza Mhe. Majaliwa.


Naibu Waziri wa  Ujenzi na Uchukuzi Mhe. Mhandisi Godfrey Kasekenya amesema  meli hiyo n kama haitakuwa na changamoto itakabidhiwa kwa wahusika ambao ni Kampuni ya Huduma za Meli Tanzania (MSCL) kwa ajili ya kuanza kuiendesha.

“Sifa za meli hii itakuwa na uwezo wa kubeba abiria 1200, tani 400 za mizigo, itakuwa na madaraja sita, itaweza kubeba viongozi wakuu wa kitaifa wawili, VIP nne,  first class 60, business class 100, second class 200 lakini pia itakuwa na wasafiri wa kawaida kama 834, inaukumbi wenye uwezo wa kubeba watu 400 ambao wanaweza kufanyia sherehe humo kwa hivyo itakuwa ni kivutio kizuri sana na itafanya safari zake katika nchi zote ambazo ziko ukanda wa ziwa viktoria,"amesema Mhe, Kasekenya.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.