• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa Majaliwa kufanya ziara ya siku nne Mwanza

Posted on: October 13th, 2022


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (MB) anatarajiwa kuwasili Mkoani Mwanza Jumamosi ya Oktoba 15, 2022 Majira ya saa 10 jioni kwa ziara ya kikazi.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Kighoma Malima wakati wa Mkutano na Waandishi wa Habari uliofanyika kwenye Ukumbi wa Ofisi ya Mkoa  mapema leo alhamisi Oktoba 13, 2022.

Mhe. Malima ametumia wasaa huo kuwakaribisha wananchi wa Mwanza na Mikoa ya jirani kujitokeza kwa wingi kandokando ya barabara na kwenye Miradi atakayoitembelea kumlaki na kumpokea Kiongozi huyo ambaye atakuwepo mkoani humo kwa ziara ya siku nne.

"Nawaomba wakaazi wa Mwanza tuoneshe uzalendo wa dhati, sote tuungane kumpokea Mgeni wetu na tumwoneshe mapenzi ya dhati huku tukiishukuru Serikali kwa kutuletea Maendeleo kama tunavyoona Miradi mbalimbali inaendelea kutekelezwa kwenye maeneo yetu." Mkuu wa Mkoa.

Akizungumzia ratiba ya ziara amesema ,siku ya jumapili ya Oktoba 16, 2022 kuanzia Majira ya saa 2 asubihi Mhe. Majaliwa atakagua Maendeleo ya Ujenzi wa Daraja la Magufuli Kigongo-Busisi pamoja na kusalimia wananchi wa Busisi kabla ya kuelekea wilayani Kwimba ambako atakagua Maendeleo ya Ujenzi wa Mradi wa Reli ya kisasa (SGR).

Malima amefafanua kuwa katika siku hiyohiyo, kuanzia Majira ya saa 7 mchana Mhe. Waziri Mkuu atazindua Jengo la Huduma ya Macho kwenye Hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando pamoja na kuzungumza na  wananchi kwenye uwanja wa Mahafali hospitalini hapo.

"Siku ya tatu ya ziara ya Mhe. Waziri Mkuu itaanzia Wilayani Ukerewe kwenye visiwa vya Irugwa majira ya saa 3 asubuhi ambako atakagua ujenzi wa Kituo cha Afya na Maendeleo ya Shule ya Sekondari ya Irugwa kabla ya kuelekea kisiwani Gana ambako akiwa huko atakagua maendeleo ya Ujenzi wa Zahanati pamoja na kusalimia wananchi." Amesema Mhe. Malima.

Ameongeza kuwa mara baada ya shughuli za visiwani Mhe. Waziri Mkuu atarejea Mjini Mwanza ambako anatarajiwa kukagua Maendeleo ya Ujenzi wa Stendi ya Mabasi ya Nyegezi kuanzia Majira ya saa 9 alasiri na baadae atawasili bandari ya Mwanza Kusini kwa ajili ya kukagua maendeleo ya Ujenzi wa Meli ya MV Mwanza 'Hapa Kazi Tu'.

Awali amefafanua kuwa Mkandarasi anayejenga Barabara za Mjini Ukerewe kwa kiwango cha Lami Nyepesi kuikamilisha ifikapo Oktoba 15, 2022 kama alivyoagiza alipofanya ziara wilayani humo mwezi uliopita na ametoa wito kwa watumiaji wa Vyombo vya Moto kuziangatia Sheria za Usalama Barabarani ili kuwalinda watumiaji na kujiepusha na ajali.  

Vilevile, Mkuu wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza Kamishna Mwandamizi Msaidizi Ramadhani Ng'anzi amesema jeshi hilo pamoja na mambo mengine litahakikisha katika barabara zote zinazoingia Mkoa wa Mwanza hakutakua na Chombo cha Moto kitakachoharibika na kubaki bila kushughulikiwa kwani tabia hiyo imekua ikisababisha ajali na watembea kwa miguu watapewa uangalizi maalumu ili kuwalinda na ajali za Barabarani.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.