• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

ZAIDI YA WANANCHI ELFU 3 WAPATA MAJI SAFI NA SALAMA MURUTANGA-UKEREWE

Posted on: July 13th, 2023

ZAIDI YA WANANCHI ELFU 3 WAPATA MAJI SAFI NA SALAMA MURUTANGA-UKEREWE


Mwenge wa Uhuru umezindua Upanuzi wa Mradi wa Maji Murutanga (Tanki la Maji Kagunguli) wenye thamani ya zaidi ya Milioni 279 kutoka chanzo cha Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya Ugonjwa wa Uviko 19 wilayani Ukerewe ambao umewanufaisha zaidi ya wananchi elfu tatu.

Akizungumza baada ya Uzinduzi huo leo Julai 13, 2023, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2023 Ndugu Abdalla Shaib Kaim amewapongeza Mkuu wa Wilaya, RUWASA na Watendaji wa Ukerewe kwa ujumla kwa Usimamizi mzuri ulioleta matokeo ya mradi bora unaoendana na thamani ya fedha zilizotumika.

"Mwenge wa Uhuru 2023 umekagua Mradi huu kwa kina na itoshe tu kusema ubora umezingatiwa na hakika RUWASA mmeonesha nia ya kumuunga mkono Mhe. Rais kwa kumtua mama ndoo kichwani na kuwaletea huduma bora ya Maji wananchi." Ndugu Kaim.

Naye, Mbunge Viti Maalumu (CCM) Mhe. Furaha Matondo amesema uwepo wa huduma hiyo utasaidia kuwaondoa wananchi wa Kijiji hicho dhidi ya magonjwa ya mlipuko na tumbo kutokana na uwepo wa maji Safi kwenye makazi yao.

Mapema asubuhi Mwenge wa Uhuru ulifika kwenye Mradi wa Ufugaji Samaki ambapo kiongozi wa mbio za Mwenge ametoa rai kwa Halmashauri kuwainua vijana kwa kuwakopesha fedha kupitia fungu la asilimia 10 za mapato ya ndani ili wakuje mitaji yao na kuweza kuwapa urahisi wa kununua malighafi kama chakula na vifaranga.

Akiweka Jiwe la Msingi kwenye Ujenzi wa Kituo cha Afya Murukilima mradi unaotarajiwa kukamilika Mwezi Septemba mwaka huu kwa kupata Miundombinu yenye thamani ya zaidi ya Milioni 500, Ndugu Kaim amewapongeza kwa Usimamizi mzuri wa mradi ambao utawanufaisha zaidi ya wananchi elfu 58 kwa kupata huduma za afya karibu.

Akikagua shamba la matunda kwenye kijiji cha Gillu lililopandwa miche 2992 aina ya Machungwa na maembe, Ndugu Kaim ametoa wito kwa Mkuu wa Wilaya kufuatilia kwa karibu shamba hilo ili kuipa tija Milioni 27.7 iliyowekezwa na kwenye Madarasa 7 yaliyozinduliwa kwenye Sekondari ya Ilangala ameagiza urekebishaji wa dosari zilizobainika.

Zikihitimishwa mbio za Mwenge wa Uhuru wilayani Ukerewe kwa kukimbizwa kwenye miradi sita yenye thamani ya zaidi ya Shilingi Bilioni 1.1, Kikundi cha Vijana Ufundi ni Ajira kilihiyimisha mbio hizo kwa kushauriwa Maafisa husika kuwapa mafunzo vijana na wote wanaowakopesha ili waweze kutumia vizuri mikopo yao.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.