• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Bashe aziagiza Taasisi za kilimo,Utafiti kuhamia nanenane

Posted on: August 3rd, 2019


Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe.Hussein Bashe  amezitaka taasisi za umma na binafsi ambazo zinajihusisha na masuala ya utafiti na kilimo  kuomba eneo la kudumu katika Viwanja vya Maonyesho ya Wakulima (Nanenane- Nyamhongolo) mkoani Mwanza ili kuweka miundombinu yake ya mafunzo ya  vitendo kwa wakulima wote.


Amesema kitendo cha taasisi hizo kujitokeza siku za maonyesho pekee  hazitoshi kuwaelimisha wakulima na badala yake wanapaswa kuhamia hapo huku akiwataka kuanza harakati kwa kuihusisha  wizara ya kilimo ili kusaidia upatikanaji wa maji  eneo hilo muda wote kwa ajili ya kilimo.


Kauli hiyo ameitoa  wakati akizungumza na viongozi wa Jeshi la Magereza, Taasisi ya Kilimo Tanzania (TARI), Taasisi ya  Tanzania Horticultural Association (TAHA) inayojuhusisha na kuendeleza tasnia ya kilimo na wengineo ambapo aliwataka  kuwa na ofisi ndogo na maeneo ya kilimo, utafiti na mafunzo kwa wakulima.


“Kitendo chenu ya kuonekana siku za maonyesho hakiwezi kuwasaidia wakulima, hapa mnatakiwa kuwepo muda wote na siyo siku nane  kisha mnatoweka na kurudi maofisini,  mnatakiwa kuwa na maji ya uhakika na shughuli zenu zifanyike muda wote kama mnahitaji msaada wa wizara toeni taarifa ili tusaidiene.


“Mfano tumeona namna mazao na mbogamboga zilivyostawi katika vitalu  vya magareza na Taha, kama wakulima wote wangepata elimu na utalaamu uliotumika sidhani kama tungekuwa hapa tulipo, sasa mkikaa na utalaamu wenu ndiyo maana wakulima wanakimbia sekta hiyo kwa kuhofia kupata hasara.


“Nashukuru kuona magereza wameanza kujenga  ofisi zao hapa,  naombeni eneo hili litumike kwa kilimo hata viongozi wengine waje kujifunza hapa, kama taasisi zote za utafiti na kilimo bora zingekuwa maeneo ya kilimo bila  shaka wakulima ndio watu wa kutolea mfano kwa kipato kikubwa,”alisema.


Meneja  Mkuu Uendeshaji wa Taha, Simon Mlay alimweleza Bashe kwamba   kutokana na kulima kwa kutumia mbolea , mbegu bora na kufuata utalaam, mazao yao hukomaa ndani ya miezi miwili huku mbogamboga zikichukua siku 30 hadi 45.


Hata alisema wapo tayari kukaa eneo hilo ikiwa watapewa eneo la kujenga ofisi huku akiomba   uongozi unaohusika  na viwanja  hivyo kuweka uzio ili kuzuia mifugo  ya wananchi kuingia katika mashamba hayo.


Naye Mkuu wa Wilaya ya Chato, Mtemi Msafiri, alimuomba Bashe kwamba  watu wa Mkoa wa Geita  wanaomba kufufuliwa kituo cha utafiti cha Bwaga badala ya kutegemea cha Ukiliguru kilichopo Wilaya ya Misungwi mkoani Mwnaza.


Pia alimuomba kuwafikishia maombi yao Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA)  kuwahi kutoa taarifa za hali ya hewa ili watendaji  na wataalamu wa kilimo waweze kufikisha mapema elimu kwa wananchi.


Naye Mkuu wa Wilaya ya Sengerema, Emmanuel Kipole alisema  wameendelea na uhamasishaji wa kilimo cha mazao na malighafi ikiwa lengo ni kufikia uchumi wa kati.Aliongeza kuwa wananchi wa Sengerema na mkoa wa Mwanza wamehamasika kulima zao la pamba kutokana na jitihada zinazochukuliwa na Serikali.


Kwa upande wa Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya maonyesho ya Nanenane  yanayohusisha Mikoa ya Mwanza, Kagera na Geita alisema  kulikuwa na  washiriki 260, halmashauri 12 kati ya 22, wadau wa sekta ya kilimo 150 walikuwa wamehudhuria huku matarajio ni kuwa na wadau  350 walio rasmi.



Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.