• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

OR-UTUMISHI YATOA MAAGIZO KUTEKELEZA AFUA ZA KUDHIBITI VVU, UKIMWI, MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA

Posted on: September 8th, 2025

Leo Septemba 08, 2025 Kaimu Katibu Mkuu OR- UTUMISHI ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu wa wizara hiyo Bw. Musa Magufuli amefungua Kikao cha Kamati ya Kitaifa, Waratibu wa Wizara wa VVU, UKIMWI na Magonjwa sugu yasiyoambukiza mahali pa kazi na wajumbe wa ngazi ya Taifa na Mkoa jijini Mwanza na kutoa maagizo kadhaa.

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu wa wizara hiyo kwenye Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Bw. Magufuli amesema Wizara zina wajibu wa kusimamia ofisi za chini kutekeleza muongozo wa kuthibiti VVU, UKIMWI na Magonjwa sugu yasiyoambukiza mahala pa kazi katika utumishi wa umma (2024) pamoja na Sekretatieti za Mikoa kusimamia LGA's kutekeleza waraka namba 02.

Aidha, amesema katika kufanikisha hayo ni lazima ofisi zitoe mafunzo ya kuwajengea uwezo watumishi pamoja na kuteua na kubuisha kamati na kuteua waratibu na kuwapa vitendea kazi vya kutekeleza afua hizo huku akibainisha umuhimu wa kuhuisha takwimu na kuziwasilisha OR- UTUMISHI pamoja na kutenga bajeti ya kufanikisha.

Awali, amebainisha kuwa kwa mwaka 2025 jumla ya watumishi 1983 wamejiweka wazi kuishi na VVU na UKIMWI kutoka katika taasisi 240 ambapo 884 ni wanaume na 1099 ni wanawake na kwamba kwa kipindi cha julai 2023- Juni 2025 watumishi 18842 wamepatiwa matibabu ya Afya ya Akili katika hospitali ya Taifa Milembe wakiwemo watumishi wa umma jambo linalodhoofisha ufanisi wa utendaji kazi.

Naye, Katibu Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana amebainisha juhudi za Mkoa huo katika kukabiliana na VVU, UKIMWI na Magonjwa yasiyo ambukiza kwamba Mkoa huo umeunda kamati za kusimamia utekelezaji wa afua hizo kuanzia ngazi za kata hadi wilaya na kwamba kamati hizo zipo hai pamoja na changamoto ya bajeti finyu.

"Mtu anapokua na mgonjwa mwenye maambukizi ya UKIMWI unakosa muda wa kuzalisha mali kwa kujikita kwenye kumuuguza hivyo Mwanza tunaendelea kutoa Elimu kwa jamii kuachana na tabia hatarishi ili wananchi wawe na afya njema na kuweza kujihusisha na shughuli za usalishaji kama kilimo, uvuvi na ufugaji." Amesema Balandya.

Aidha, amempongeza Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Jesca Lebba kwa kusimamia mazoezi ya watumishi yanayofanyika mara tatu kwa juma na kwa kuongoza mbio na matembezi ya Kilomita tano kila mwezi ikiwa ni juhudi za Mkoa huo katika kuweka afya za watumishi imara na kuepuka magonjwa yasiyo ambukiza.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA AKABIDHI MAGARI YA BILIONI 1.3 KWA JESHI LA POLISI

    September 12, 2025
  • SERIKALI KUENDELEA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI NCHINI

    September 11, 2025
  • MAJALIWA AAGIZA KUIMARISHWA ZAIDI SEKTA YA UFUATILIAJI, TATHMINI NCHINI

    September 11, 2025
  • NSSF WAFANYA ZIARA YA UWEKEZAJI MWANZA

    September 10, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.